| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Somalia kuanza kutoa hati za kusafiria za Jumuiya ya Afrika Mashariki
Hatua hii ni sehemu ya kujumuisha Somalia katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Somalia kuanza kutoa hati za kusafiria za Jumuiya ya Afrika Mashariki
Somalia imekabidhi muundo wa hati ya kusafiria ya kanda ya EAC mjini Arusha, Tanzania. / Wengine

Somalia inatarajiwa kuanza kutoa hati za kusafiria za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kwa raia wake, na kuungana na nchi wanachama wengine wanaotumia pasipoti hizo.

Balozai wa Somalia nchini Tanzania na Mwakilishi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Ilyas Ali Hassan, amemkabidhi Waziri wa Mambo ya Ndani wa Somalia Jenerali Abdullahi Sheikh Ismail “Fartaag” na Mkurugenzi Mkuu wa Uhamiaji wa Somalia, Mustafa Sheikh Ahmed Dhuhulow hati yenye nembo ya Afrika Mashariki, nchini Tanzania siku ya Jumanne.

Hatua hii ni muhimu kidiplomasia kwa Somalia na inatarajiwa kuimarisha ushirikiano katika kanda na kurahisisha raia wa Somalia kufanya ziara bila vikwazo katika maeneo ya Afrika Mashariki.

Somalia imeidhinishwa kuchapisha hati za kusafiria za Afrika Mashariki Disemba 2025, kabla wiki hii kutolewa muundo wa pasipoti ulioidhinishwa.

Hati za kusafiria ya EAC ilianzishwa katika Mkutano wa 17 wa Wakuu wa Nchi za Afrika Mashariki tarehe 2 Machi, 2016, ambapo viongozi pia walianzisha pasipoti za kielektroniki katika madaraja matatu - Diplomasia, watumishi wa umma na la kawaida.

Pasipoti a elektroniki, ambazo zinatambuliwa kimataifa, zilianzishwa kuchukua nafasi ya zile za mataifa wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Wanachama wengine wa Jumuiya ya Afrika Mashariki

Kuanzishwa kwa hati hizo za kusafiria za Afrika Mashariki hatua kwa hatua kwa nchi zote wanachama kumeweka msisitizo wa kuainisha pasipoti katika kanda hiyo.

Somalia ilijiunga rasmi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kama nchi wanachama wa nane baada ya kuwasilisha nyaraka za Kuidhibishwa kw Makubaliano kwa Katibu Mkuu kwenye hafla iliyofanyika Makao Makuu ya EAC mjini Arusha, Tanzania, Machi 2024.

Hatua hii inafuatia kuidhinishwa kwa uanachama wa Somalia na viongozi wa kanda katika Mkutano wa 23 wa Wakuu wa Nchi wa EAC mjini Arusha.

Wanachama wengine ni Burundi, Kenya, Rwanda, Sudan Kusini, Tanzania, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Uganda.

Somalia tayari imeshateua wabunge tisa kwa Bunge la Afrika Mashariki (EALA), ambao watawawakilisha katika makao makuu mjini Arusha, Tanzania.

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
Ronaldo na Messi Kombe la Dunia mara ya 6
"Makubaliano makubwa" yamefikiwa na Iran: Trump
Bajeti ya trilioni 62.33 Tanzania na kupanda kwa gharama ya maisha
Raia 262 wa Nigeria wanaokimbia mashambulizi dhidi ya wageni Afrika Kusini warudishwa nyumbani
Vikosi vya Marekani na Nigeria vyawakata makali zaidi ya magaidi 200 kaskazini mashariki
Mabadiliko ya uchumi Nigeria, Uganda na nchi nyengine za Afrika yamekuza uwekezaji: Benki Kuu
Serikali ya Somalia yasikitishwa na hatua ya kuzuiwa kwa mwamuzi wa nchi hio kuingia Marekani
Watu wasiopungua 12 wauawa katika mashambulizi ya risasi jijini Johannesburg
Refa wa Somalia arudi nyumbani baada ya kukataliwa kuingia Marekani
Trump: Helikopta ya Jeshi la Marekani imedunguliwa na Iran, tutalipiza kisasi
Wakazi wa Afrika Kusini KwaZulu-Natal katika tahadhari baada ya simba kutoroka hifadhi ya wanyama
FIFA yamuondoa mwamuzi kutoka somalia Artan katika Kombe la Dunia baada ya kuzuiwa kuingia Marekani
Waandamanaji wanaopinga kujengwa kwa kituo cha Marekani cha Ebola wakamatwa nchini Kenya
Mwendesha Mashtala wa ICC asimamishwa kazi kwa madai ya dhulma za ngono
Mahakama Kuu ya Kenya: Mchakato wa kumuondoa Gachagua madarakani ulifuata Sheria
Mwamuzi wa kwanza wa Somalia aliyetarajiwa kuchezesha  Kombe la Dunia azuiwa kuingia Marekani
Uhamiaji: Afrika Kusini kuhamisha vituo vya wakimbizi hadi maeneo ya mpakani
Davido, Burna Boy, Rema na Tyla kutumbuiza Kombe la Dunia 2026
Mauritius yakataa pendekezo lililoripotiwa la Marekani la kununua Visiwa vya Chagos
Wananchi waelimishwe kuhusu umuhimu wa kuandikishana mikataba ya ardhi-Wazri Mkuu wa Tanzania