| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Rais wa Djibouti Guelleh awasilisha ombi la kugombea muhula wa sita
Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 77 anaruhusiwa kugombea tena baada ya bunge bunge mwaka jana kuondoa ukomo wa umri kikatiba kwa wagombea urais.
Rais wa Djibouti Guelleh awasilisha ombi la kugombea muhula wa sita
Rais Ismail Omar Guelleh amekuwa madarakani tangu 1999. / AA

Rais wa Djibouti Ismail Omar Guelleh, ambaye amekuwa madarakani tangu 1999, amewasilisha rasmi ombi la kugombea muhula wa sita katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwezi Aprili, kulingana na Wizara ya Mambo ya Ndani.

Ombi la Guelleh liliwasilishwa siku ya Jumatatu na mkurugenzi wa kampeni yake, Abdallah Abdillahi Miguil, ambaye ni mwanachama mwandamizi wa Muungano unaoongoza serikali, UMP.

Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 77 anaruhusiwa kugombea tena baada ya bunge mwaka jana kuondoa ukomo wa umri kikatiba kwa wagombea urais.

Katiba ilikuwa tayari imebadilishwa 2010 kuondoa sheria ya mihula miwili pekee kwa urais.

Guelleh anagombea tena urais kupitia muungano wa vyama kadhaa vya kisiasa ambavyo vinaunga mkono serikali.

Mamlaka za Uchaguzi zinatarajiwa kutathmini maombi hayo kabla ya kutangaza orodha ya mwisho ya wagombea wanaoruhusiwa kwenye uchaguzi.

Kampeni za uchaguzi zinatarajiwa kuanza katika wiki chache zijazo.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Ronaldo na Messi Kombe la Dunia mara ya 6
"Makubaliano makubwa" yamefikiwa na Iran: Trump
Bajeti ya trilioni 62.33 Tanzania na kupanda kwa gharama ya maisha
Raia 262 wa Nigeria wanaokimbia mashambulizi dhidi ya wageni Afrika Kusini warudishwa nyumbani
Vikosi vya Marekani na Nigeria vyawakata makali zaidi ya magaidi 200 kaskazini mashariki
Mabadiliko ya uchumi Nigeria, Uganda na nchi nyengine za Afrika yamekuza uwekezaji: Benki Kuu
Serikali ya Somalia yasikitishwa na hatua ya kuzuiwa kwa mwamuzi wa nchi hio kuingia Marekani
Watu wasiopungua 12 wauawa katika mashambulizi ya risasi jijini Johannesburg
Refa wa Somalia arudi nyumbani baada ya kukataliwa kuingia Marekani
Trump: Helikopta ya Jeshi la Marekani imedunguliwa na Iran, tutalipiza kisasi
Wakazi wa Afrika Kusini KwaZulu-Natal katika tahadhari baada ya simba kutoroka hifadhi ya wanyama
FIFA yamuondoa mwamuzi kutoka somalia Artan katika Kombe la Dunia baada ya kuzuiwa kuingia Marekani
Waandamanaji wanaopinga kujengwa kwa kituo cha Marekani cha Ebola wakamatwa nchini Kenya
Mwendesha Mashtala wa ICC asimamishwa kazi kwa madai ya dhulma za ngono
Mahakama Kuu ya Kenya: Mchakato wa kumuondoa Gachagua madarakani ulifuata Sheria
Mwamuzi wa kwanza wa Somalia aliyetarajiwa kuchezesha  Kombe la Dunia azuiwa kuingia Marekani
Uhamiaji: Afrika Kusini kuhamisha vituo vya wakimbizi hadi maeneo ya mpakani
Davido, Burna Boy, Rema na Tyla kutumbuiza Kombe la Dunia 2026
Mauritius yakataa pendekezo lililoripotiwa la Marekani la kununua Visiwa vya Chagos
Wananchi waelimishwe kuhusu umuhimu wa kuandikishana mikataba ya ardhi-Wazri Mkuu wa Tanzania