| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Mkataba wa Ulinzi wa Makkah waweka msingi wa kujenga mfumo mpya wa usalama wa kikanda: Fidan
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, amesema kuwa muungano wa nchi hizo tatu unalenga kupanua ushirikiano, kupunguza hali ya sintofahamu na kuimarisha utulivu katika eneo hilo.
Mkataba wa Ulinzi wa Makkah waweka msingi wa kujenga mfumo mpya wa usalama wa kikanda: Fidan
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, anasema muungano huo utasaidia kuimarisha utulivu wa kikanda na kupunguza hali ya kutokuwa na uhakika. / / AA

Mkataba wa Pamoja wa Ulinzi wa Makkah umeanzisha mchakato wa kujenga “mfumo mpya wa usalama na ushirikiano” katika eneo hilo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Hakan Fidan, amesema.

Akizungumza mjini Istanbul siku ya Jumatatu, baada ya mkutano wa kwanza wa Kamati ya Kimkakati ya Kisiasa na Ulinzi iliyoundwa chini ya mkataba huo, Fidan amesema muungano huo utasaidia kuimarisha utulivu wa kikanda na kupunguza hali ya sintofahamu.

“Kwa muungano huu, tutaona utulivu mkubwa ukijengeka hatua kwa hatua katika eneo hili, huku hali ya sintofahamu ikipungua,” Fidan amesema.

Mkataba huo unaziunganisha Uturuki, Saudi Arabia na Pakistan katika mfumo wa karibu zaidi wa ushirikiano wa kiulinzi, wakati hali ya usalama katika eneo hilo ikiendelea kubadilika.

‘Netanyahu ni adui wa ubinadamu’

Fidan amesema Muungano wa Ulinzi wa Makkah “umeanzishwa kwa lengo la kupanuliwa,” akionyesha kuwa Uturuki inaona mfumo huo kuwa msingi wa kupanua ushirikiano wa kikanda.

Amesema kamati hiyo mpya itakuwa na jukumu la kuendeleza ajenda ya kisiasa na kiulinzi ya muungano huo.

Fidan pia ameulizwa kuhusu kauli za hivi karibuni kutoka kwa serikali ya Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, ambazo zimekuwa zikiiwasilisha Uturuki kama tishio la kimkakati.

“Netanyahu, ambaye amekuwa adui wa ubinadamu, jumuiya ya kimataifa na usalama, si mtu anayepaswa kuchukuliwa kwa uzito,” Fidan alisema.

“Mfumo wa kimataifa lazima upambane na tishio la Netanyahu,” aliongeza.

CHANZO:TRT World and Agencies