| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Uturuki, Pakistan na Saudi Arabia kufanya mkutano wa kwanza wa makubaliano ya ulinzi ya Makka
Kwa mujibu wa vyanzo vya wizara ya mambo ya nje, mkutano huo unatarajiwa kuhudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan, Waziri wa Ulinzi Yasar Guler na Mkuu wa Majeshi Jenerali Selcuk Bayraktaroglu.
Uturuki, Pakistan na Saudi Arabia kufanya mkutano wa kwanza wa makubaliano ya ulinzi ya Makka
Uturuki, Pakistan na Saudi Arabia zilitia saini mkataba wa ulinzi mnamo tarehe 7 Agosti. / Picha: Akiba ya Reuters

Mkutano wa kwanza wa Kamati ya Kimkakati, Siasa na Ulinzi iliyoundwa chini ya Makubaliano ya Pamoja ya Ulinzi ya Mekkah utafanyika jijini Istanbul Jumatatu.

Kwa mujibu wa vyanzo vya wizara ya mambo ya nje, mkutano huo unatarajiwa kuhudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan, Waziri wa Ulinzi Yasar Guler na Mkuu wa Majeshi Jenerali Selcuk Bayraktaroglu.

Pakistan inatarajiwa kuwakilishwa na Waziri wa Mambo ya Nje Mohammad Ishaq Dar, Waziri wa Ulinzi Khawaja Muhammad Asif na Mkuu wa Majeshi Asim Munir, huku Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudi Arabia Faisal bin Farhan, Waziri wa Ulinzi Khalid bin Salman na Mkuu wa Majeshi Jenerali Fayyadh bin Hamed Al-Ruwaili wakitarajiwa kuhudhuria.

Kamati, inayojumuisha mawaziri wa mambo ya nje na ulinzi pamoja na wakuu wa majeshi wa Uturuki, Pakistan na Saudi Arabia, inatarajiwa kutoa mwelekeo wa kimkakati wa shughuli zitakazoendeshwa chini ya Makubaliano ya Pamoja ya Makkah.

Mkutano huo unatarajiwa kugusia changamoto za kimataifa za kiusalama, pamoja na jitihada za kujenga uwezo wa ulinzi na kukuza ushirikiano wa vikosi vya nchi hizo tatu.

Washiriki pia wanatarajiwa kujadili ushirikiano wa kina katika ulinzi, ikiwemo uzalishaji wa pamoja, utafiti na maendeleo, pamoja na kukuza jitihada za pamoja za kukabiliana na ugaidi.

Mkutano huo pia unatarajiwa kutoa ramani ya sekretariati na mambo mengine yatakayoongoza katika maeneo ya pamoja yanayodhamiriwa na Kamati ya Kimkakati ya Ulinzi na Siasa, pamoja na muongozo wa hatua za kuchukuliwa katika siku zijazo.

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan, Mwanamfalme wa Saudi Arabia Mohammed bin Salman na Waziri Mkuu wa Pakistan Shehbaz Sharif walisaini Makubaliano ya Ulinzi wa Pamoja ya Makkah Agosti 7.

Makubaliano hayo yalihusu uwajibikaji wa pamoja wa kikanda wakati kukiwa na ongezeko la kukosekana kwa utulivu katika maeneo yao na kimataifa, makubaliano hayo yanalenga kukuza ulinzi, amani, utulivu na maendeleo ya kikanda na kimataifa.

Makubaliano hayo yanasema shambulio dhidi ya mjumbe yeyote litaangaliwa kama shambulio dhidi ya wajumbe wote.

Likiwa na lengo la kuweka ushirikiano mpya wa kikanda, makubaliano hayo yanaruhusu ushiriki wa wajumbe ambao wanaheshimu sheria za kimataifa na kuwa na maono ya ushirikiano wa kuleta amani.

CHANZO:َAA