| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Tanzania, Misri ruksa raia wake kuingia Sudan Kusini bila viza
Kwa mujibu wa taarifa hiyo mpya, ni nchi mbili pekee ambazo zimeongezwa katika orodha ya raia wake kuruhusiwa kuingia bila viza nchini Sudan Kusini, nazo ni Misri na Tanzania.
Tanzania, Misri ruksa raia wake kuingia Sudan Kusini bila viza
Tanzania na Misri zimeingia katika orodha ya nchi zinazoruhusiwa kuingia Sudan Kusini bila viza.

Serikali ya Sudan Kusini imetoa orodha mpya ya sera za viza ambapo imeiorodhesha Tanzania na Misri miongoni mwa nchi ambazo raia wake wanaruhusiwa kuingia bila viza au kulipia viza.

Muongozo huo mpya unatoa taarifa zaidi ya vigezo vinavyohitajika kwa wasafiri kutoka mataifa ya Afrika na sehemu nyengine ya dunia.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo mpya, ni nchi mbili pekee ambazo zimeongezwa katika orodha ya raia wake kuruhusiwa kuingia bila viza nchini Sudan Kusini, nazo ni Misri na Tanzania.

Hata hivyo, raia kutoka mataifa mengine ya Afrika, ikiwemo Ghana na Nigeria hawapo katika orodha hiyo.

Tanzania na Misri, zinaungana na Kenya ambayo pia raia wake wenye hati sahihi ya kusafiria, wanaruhusiwa kuingia nchini Sudan Kusini bila viza wala malipo ya viza. Utaratibu huo ulianza Julai 28, 2021.