Algeria imetangaza kusitisha uhusiano wake wa kidiplomasia na Umoja wa Falme za Kiarabu, na kusema imetumia njia zote za kudumisha uhusiano kati ya nchi hizo mbili.
Uamuzi huo ulitangazwa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Algeria, kwa mujibu wa taarifa rasmi ya Shirika la Habari la Algeria (APS).
"Algeria imeamua siku ya Alhamisi kusitisha uhusiano wake wa kidiplomasia na UAE baada ya kutumia njia zote za kudumisha uhusiano kati ya nchi mbili, kwa mujibu wa Wizara ya Mambo ya Nje," imeandika APS.
Wizara haikutoa taarifa zaidi ya sababu ya kuchukua uamuzi huo.
Hatua hiyo inaonesha kuendelea kuzorota kwa mahusiano kati ya nchi hizo mbili za Kiarabu.
ZILIZOPENDEKEZWA



















