Wake wa Marais wa Afrika: Entissar Amer wa Misri
Entissar Amer ni mke wa rais wa Misri/ Picha:EgyptToday / Public domain
Wake wa Marais wa Afrika: Entissar Amer wa Misri
Entissar alifunga ndoa na Abdel Fattah el-Sisi mwaka 1977, baada ya el Sisi kuhitimu kutoka Chuo cha Kijeshi.

Entissar Amer ndie mke wa Rais wa Misri.

Amekuwa mke wa Rais wa nchi hiyo tangu Juni 2014, wakati mume wake, Abdel Fattah el-Sisi, alipokuwa Rais wa Misri.

Entissar Amer alizaliwa Disemba 3, 1956. Ana shahada ya kitaaluma katika biashara, akibobea katika uhasibu.

Entissar alifunga ndoa na Abdel Fattah el-Sisi mwaka 1977, baada ya el Sisi kuhitimu kutoka Chuo cha Kijeshi.

Ingawa wake wa kwanza wa marais wa Misri mara nyingi walikuwa na majukumu yanayoonekana sana ya kisiasa na kisheria, Entissar Amer kwa ujumla hudumisha wasifu wa kitamaduni, unaozingatia haki za wanawake, ustawi wa watoto, na uhifadhi wa kitamaduni.

Anazingatia sana miradi ya usaidizi wa raia wasiojiweza, maendeleo ya jamii, na uwezeshaji wa wanawake. Mara kwa mara anawakilisha taifa katika hafla muhimu za kidiplomasia na kitamaduni.

Pia anaiwakilisha Misri wakati wa ziara za kidiplomasia za hali ya juu, kwa kuwakaribisha wageni mashuhuri.

Kama mke wa Rais, mara kwa mara yeye hutetea mashirika ya kiraia na ya kibinadamu.

Kwa mfano, yeye ni mlezi wa Hilali Nyekundu ya Misri.

Chini ya ufadhili wake wa moja kwa moja, mradi wa afya uitwao "Kwa mikono yako, Unaweza kuokoa maisha” kwa ushirikiano na Wizara ya Mshikamano wa Kijamii hutoa mafunzo kwa maelfu ya wafanyakazi wa afya ya jamii.

Entissar pia anaunga mkono kikamilifu mpango wa kitaifa wa ‘Decent Life Initiative’ ambao unalenga kuwainua watu wasiojiweza katika vijiji.

Mradi huo unalenga uwezeshaji wa kijamii na kiuchumi kwa mayatima, watoto, na wanawake wasiojiweza.

Entissar Amer na Rais Abdel Fattah el-Sisi wana watoto wanne.

CHANZO:TRT Swahili