| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Rais wa Tanzania amteua binti na mkwe wake katika Baraza la Mawaziri
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amemteua binti yake, Wanu Hafidh Ameir, kuwa Naibu Waziri wa Elimu. Hafidh Ameir, mwenye umri wa miaka 43, ni Mbunge wa Jimbo la Makunduchi.
Rais wa Tanzania amteua binti na mkwe wake katika Baraza la Mawaziri
Mohamed Mchengerwa ni Mbunge wa Jimbo la Rufiji. / / Wengine

Alifanikiwa kutetea nafasi yake katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Wakati huohuo, Rais Suluhu Hassan amemteua Mohamed Mchengerwa, mume wa Hafidh Ameir, kuwa Waziri wa Afya. Mchengerwa, mwenye umri wa miaka 46, ni Mbunge wa Jimbo la Rufiji.

Mtoto wa Rais wa zamani apewa nafasi serikalini

Mtoto wa Rais wa zamani wa Tanzania, Jakaya Kikwete, naye anaonekana katika orodha ya wajumbe wapya wa serikali, Ridhwani Kikwete, ameteuliwa kuwa waziri katika Ofisi ya Rais.

Atakuwa anasimamia Utumishi wa Umma na Utawala Bora. Ridhwani, mwenye umri wa miaka 46, pia ni Mbunge wa CCM anayewakilisha Jimbo la Chalinze.

Katika mabadiliko hayo ya serikali, Rais Suluhu Hassan – aliyeshinda uchaguzi wa Oktoba 29 kwa karibu asilimia 98 ya kura – ametangaza baraza jipya lenye mawaziri 27 na manaibu waziri 29.

Waliopigwa kalamu

Viongozi saba waandamizi waliokuwa kwenye baraza la mawaziri la awali wamekosa nafasi katika baraza hilo jipya. Miongoni mwao ni aliyekuwa Waziri wa Nishati, Doto Biteko, Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe, na Waziri wa Biashara, Seleman Jafo.

Katika serikali mpya:

Khamis Musa Omar ataongoza Wizara ya Fedha.

Mahmoud Thabit Kombo ameendelea kushika nafasi ya Waziri wa Mambo ya Nje.

Prof. Riziki Shemdoe atakuwa Waziri wa Elimu, akisaidiwa na naibu wake mpya, Wanu Hafidh Ameir.

Daniel Chongolo ataongoza wizara ya kilimo.

Judith Kapinga atakuwa Waziri wa Viwanda na Biashara.

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
Algeria yasitisha uhusiano wake wa kidiplomasia na UAE
Ufalme wa Uganda wamteua mtangazaji wa televisheni kumrithi Mfalme Oyo Nyimba
Mufti Mkuu Tanzania atoa wito kwa Waislamu kufunga siku tatu kuomba kuepushwa na madhara ya El Nino
Umoja wa Mataifa wapongeza makubaliano ya Libya kuelekea katika uchaguzi
Putin amuambia Trump: Urusi haina nia ya kuzishambulia nchi za Ulaya
Wahamiaji zaidi ya 1,000 waokolewa pwani ya Afrika magharibi ndani ya wiki moja, MSF inasema
Ghana yasema imetumia $4.37 milioni kuwarudisha raia wake nyumbani kutoka Afrika Kusini
Waburundi waomba nyaraka za kusafiria kufuatia operesheni dhidi ya wafanyabiashara wa kigeni Kenya
Watu wawili wafariki, wengine 25 wajeruhiwa baada ya basi la mahujaji wa Misri kupata ajali Makkah
Mume wa Rais Samia wa Tanzania afariki dunia
Cabo Verde yatangaza maombolezo ya kitaifa baada ya vifo vya watoto katika ajali ya basi
Mlipuko wa kipindupindu, Kordofan Magharibi umesababisha vifo vya watu 23
Romanda Hombir wa Afrika Kusini ashinda taji la Miss World Africa 2026
DRC inachunguza ajali mbaya ya moto katika sherehe ya harusi ulioua wageni 22
Unyanyasaji kwa wazee janga linaloenea kimya kimya
Marekani kuondoa ufadhili wa Dola milioni 45 za VVU kwa Namibia
Niger yaishutumu Ufaransa kwa jaribio lililofeli la uasi wa kijeshi
Huduma ya Kitaifa ya Polisi ya Kenya (NPS) inatoa onyo kwa wanasiasa kabla ya uchaguzi mkuu
Marekani yaongeza muda wa AGOA hadi mwisho wa 2028
Marekani inashinikiza kusitishwa kwa mapigano kwa sababu za kibinadamu bila vikwazo nchini Sudan