| Swahili
MICHEZO
1 dk kusoma
Ufaransa yapenya kwa tabu dhidi ya Paraguay kutinga robo fainali ya Kombe la Dunia.
Baada ya kuifunga Paraguay bao 1-0, Ufaransa itakutana na Morocco kuwania nafasi katika nusu-fainali.
Ufaransa yapenya kwa tabu dhidi ya Paraguay kutinga robo fainali ya Kombe la Dunia.
Mbappe akishangilia kufunga bao la ushindi la Ufaransa dhidi ya Paraguay. / Ramaphosa / Ramaphosa

Ufaransa imeishinda Paraguay 1-0 na kufika robo fainali ya Kombe la Dunia, na kujitengea mpambano na Morocco.

Mshambuliaji Kylian Mbappe alifunga bao la ushindi la Ufaransa dakika ya 70 kwa mkwaju wa penalti baada ya Ufaransa kupoteza nafasi nyingi katika mchezo mzima.

Les Blues walitawala vipindi virefu vya mechi, lakini ulinzi wa Paraguay ulibaki imara hadi mchezaji mbadala Desire Doue alipoangushwa na Diego Gomez wakati wa mbio za kuingia kwenye eneo la hatari.

Bao hilo lilikuwa la saba kwa Mbappe katika Kombe la Dunia, na kumfanya awe sawa na Lionel Messi wa Argentina kama mfungaji bora wa mashindano.

Baada ya kuishinda Paraguay, Ufaransa itakabiliana na Morocco kwa nafasi katika nusu fainali ya Kombe la Dunia.

CHANZO:TRT World