Kundi la misaada la Sudan Jumapili liliripoti vifo 30 kutokana na mlipuko wa kipindupindu katika jimbo la Kordofan magharibi tangu Juni 20.
Katika taarifa, Chumba cha Dharura cha Dar Hamar kilisema watu 800 pia wameambukizwa ugonjwa huo katika kipindi hicho hicho.
Shirika hilo lilisema mlipuko huo ulirekodiwa katika maeneo ya Wad Banda na Al Nahud pamoja na vijiji jirani katika jimbo hilo.
"Takwimu hadi sasa zinaonyesha vifo 30 na maambukizi 800 ya kipindupindu katika zaidi ya vijiji 25," ilisema, ikiziomba mashirika ya kibinadamu na mamlaka za afya kuingilia kati haraka ili kutoa dawa, majimaji ya mishipa, na vifaa vya matibabu vinavyohitajika kudhibiti janga hilo.
Vita hatari
Siku ya Jumanne, wizara ya afya ya Sudan ilisema kwamba maambukizi 911 ya kipindupindu, yakiwa ni pamoja na vifo 127, viliripotiwa huko Kordofan Magharibi na Kaskazini.
Sudan imekumbwa na migogoro tangu Aprili 2023, wakati mapigano yalipozuka kati ya jeshi na Kikosi cha Usaidizi wa Haraka (RSF) kuhusu mipango ya kuunganisha kikosi cha kijeshi katika jeshi.
Vita hivyo vimesababisha moja ya migogoro mibaya zaidi ya kibinadamu duniani, na kuua makumi ya maelfu na kuwafanya watu karibu milioni 13 kuhama makazi yao.
AFRIKA
1 dk kusoma
Mlipuko wa kipindupindu waua watu 30 katika jimbo la Kordofan Magharibi nchini Sudan
Shirika la misaada la Sudan limeripoti vifo 30 kutokana na mlipuko wa kipindupindu katika jimbo la Kordofan Magharibi, tangu tarehe 20 Juni.
Soma zaidi




















