Kiungo wa Ghana, Thomas Partey, hataichezea timu yake katika mechi dhidi ya Panama siku ya Jumatano baada ya ombi lake la viza ya kuingia Canada kukataliwa, kwa mujibu wa FIFA siku ya Ijumaa.
“FIFA inaweza kuthibitisha kwamba mchezaji Thomas Partey hataweza kusafiri kutoka kambi ya timu ya Ghana iliyoko Boston, Marekani, kwenda Canada kwa ajili ya mechi yao ya kwanza dhidi ya Panama siku ya Jumatano, tarehe 17 Juni, kwa sababu ombi lake la viza limekataliwa na serikali ya Canada,” FIFA ilisema katika taarifa yake kwa shirika la habari la Reuters.
“FIFA haihusiki na taratibu za uhamiaji za nchi mwenyeji, ikiwa ni pamoja na maamuzi kuhusu utoaji wa viza.”
Partey mwenye umri wa miaka 32, aliwahi kuchezea timu ya Arsenal, sasa anachezea timu ya Villarreal ya Hispania, anakabiliwa na madai ya ubakaji na unyanyasaji wa kingono nchini Uingereza. Hata hivyo Partey amekana madai hayo.

















