| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Israel inatumia usalama kama kisingizio cha kunyakua 'ardhi zaidi': Waziri Fidan
Israel inafuatilia "ukaaji wa walowezi" kutoka maeneo ya Palestina kuelekea Lebanon na Syria, anasema mwanadiplomasia mkuu wa Uturuki.
Israel inatumia usalama kama kisingizio cha kunyakua  'ardhi zaidi': Waziri Fidan
Viongozi wa dunia na maafisa wakuu wa serikali wamekutana mjini Türkiye kuanzia Ijumaa hadi Jumapili kwa Jukwaa la Diplomasia la Antalya. / AA / AA

Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki Hakan Fidan alisema kuwa Israel inatumia usalama kama kisingizio cha kupata "ardhi zaidi".

"Israel haifuati usalama wake yenyewe. Israel inatafuta ardhi zaidi. Usalama unatumiwa na serikali ya Netanyahu kama kisingizio cha kutwaa ardhi zaidi," Fidan aliambia Jukwaa la Diplomasia la Antalya Jumamosi.

"Israel imezua udanganyifu kimataifa, ikidai kuwa Israel inapendelea usalama wake, lakini imekuwa wazi sana, haswa katika miaka ya hivi karibuni ... ni zaidi ya hapo," Fidan alisema.

Alisema kutoka ardhi ya Palestina, Gaza, Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu, Jerusalem Mashariki, na sasa kuelekea Lebanon na Syria, ni "utapakaaji wa walowezi haramu na upanuzi katika eneo hilo."

"Nadhani hii lazima ikome," Fidan alisema.

"Israel inapaswa kujua kwamba njia pekee ya kuishi kwa amani katika kanda ... ni kuziacha nchi nyingine zifurahie usalama wao wenyewe, na uadilifu wa eneo, na uhuru, kutotumia mamlaka katika nchi hizo," aliongeza.

Viongozi wa dunia na maafisa wakuu wa serikali wamekutana mjini Uturuki kuanzia Ijumaa hadi Jumapili kwa ajili ya Jukwaa la Diplomasia la Antalya - mkutano mkubwa wa kimataifa katika mji wa kusini mwa Mediterania uliolenga mwaka huu katika kudhibiti hali ya kutokuwa na uhakika duniani.

Kongamano hilo litakalofanyika chini ya usimamizi wa Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan na kuandaliwa na Wizara ya Mambo ya Nje, litakuwa na mada ya "Kuweka Ramani ya Kesho, Kusimamia Mashaka."

CHANZO:TRT World
Soma zaidi
Fidan wa Uturuki akutana na mawaziri w mambo ya nje wa Misri, Pakistan na Saudi Arabia
Erdogan aonya kuhusu migogoro ya dunia, ataka diplomasia, utulivu wa kikanda
Viongozi mbalimbali wahudhuria Jukwaa la Kidiplomasia la Antalya
Spika wa Bunge la Uturuki ataka Israel iondolewe Umoja wa Mataifa
Erdogan atuma salamu za rambirambi kufuatia shambulio la risasi shuleni katika jimbo la kusini
Erdogan wa Uturuki na Carney wa Canada wamejadili uhusiano wa mataifa mawili na masuala ya kimataifa
Fidan wa Uturuki na mwenzake wa Pakistan wajadili mazungumzo yanayoendelea kati ya Marekani na Iran
Fidan na Araghchi wamejadili kuhusu mazungumzo yanayoendelea kati ya Iran na Marekani
Erdogan wa Uturuki na Waziri Mkuu mteule wa Hungary Magyar wajadili uhusiano wa mataifa mawili
Israel inaweza kuiangazia Uturuki kama adui baada ya Iran: Mwanadiplomasia mwandamizi wa Uturuki
Viongozi wa dunia wanakusanyika Uturuki katika Mkutano wa 5 wa Diplomasia wa Antalya
Uturuki yamshutumu Netanyahu kuhusu matamshi yake yanayomlenga Rais Erdogan
Erdogan, Macron wanajadili kuhusu mapatano ya Iran, Lebanon, Gaza
Uchimbaji mafuta wa Somalia: Rais Mohamud anaipongeza Uturuki kama mshirika 'anayetegemewa'
Shirika la ndege la Uturuki lapata Afisa Mtendaji Mkuu mpya
Meli ya Uturuki ya kuchimba mafuta baharini yawasili Somalia kwa operesheni ya kwanza nje ya nchi
“NATO inapaswa ‘kubadilika’ ili kukabiliana na changamoto za vita vya kisasa: Burhanettin Duran
Erdogan: Tumenuia kuwa kati ya nchi 10 bora kwenye mauzo ya zana za ulinzi
Uturuki yaadhimisha miaka 106 ya shirika la habari la Anadolu
Rais wa Uturuki atoa salamu za Pasaka kwa jamii ya Wakristo