| Swahili
UTURUKI
1 dk kusoma
Viongozi mbalimbali wahudhuria Jukwaa la Kidiplomasia la Antalya
Uturuki ni mwenyeji wa mkutano wa 5 wa Jukwaa la Kidiplomasia la Antalya ambalo linahusisha zaidi ya nchi 150 duniani.
Viongozi mbalimbali wahudhuria Jukwaa la Kidiplomasia la Antalya
Zaidi ya mataifa 150 yanahudhuria jukwaa hilo, wakiwemo zaidi ya wakuu wa nchi zaidi 20./Picha:AA

Mkutano wa 5 wa Jukwaa la Kidiplomasia la Antalya umeanza siku ya Ijumaa nchini Uturuki, ukiwaleta pamoja viongozi mbalimbali duniani kuzungumzia hali ya sasa ulimwenguni.

Likiwa limeandaliwa na Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki, jukwaa hilo la siku tatu linafanyika katika mji wa kitalii wa Antalya, chini ya kauli mbiu Maandalizi ya Kesho, Kutatua Wasiwasi.

Zaidi ya mataifa 150 yanahudhuria jukwaa hilo, wakiwemo zaidi ya wakuu wa nchi zaidi 20.

Jukwaa hilo, pia linawaleta pamoja zaidi ya mawaziri 50, na wawakilishi kutoka mashirika 75 ya kimataifa.

Kwa ujumla, zaidi ya washiriki 5,000 wanatarajiwa kuhudhuria tukio hilo, huku nusu yao wakitokea Afrika na Ulaya.

Mawaziri wa mambo ya nje kutoka Afrika, Ulaya na Asia wanatarajiwa kuhudhuria jukwaa hilo.

Kutakuwa na zaidi ya majopo 40 wakati wa jukwaa hilo, ambao yatahusisha mijadala kuhusu uongozi, uchumi, mazingira, siasa na teknolojia.

Mijadala hiyo itarushwa moja kwa moja kupitia tovuti na mitandao ya kijamii, pamoja na choombo cha habari cha TRT.

Wakati wa jukwaa hilo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan anatarajiwa kuhudhuria vikao tofauti, ikiwemo cha Gaza.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Israel inatumia usalama kama kisingizio cha kunyakua  'ardhi zaidi': Waziri Fidan
Fidan wa Uturuki akutana na mawaziri w mambo ya nje wa Misri, Pakistan na Saudi Arabia
Erdogan aonya kuhusu migogoro ya dunia, ataka diplomasia, utulivu wa kikanda
Spika wa Bunge la Uturuki ataka Israel iondolewe Umoja wa Mataifa
Erdogan atuma salamu za rambirambi kufuatia shambulio la risasi shuleni katika jimbo la kusini
Erdogan wa Uturuki na Carney wa Canada wamejadili uhusiano wa mataifa mawili na masuala ya kimataifa
Fidan wa Uturuki na mwenzake wa Pakistan wajadili mazungumzo yanayoendelea kati ya Marekani na Iran
Fidan na Araghchi wamejadili kuhusu mazungumzo yanayoendelea kati ya Iran na Marekani
Erdogan wa Uturuki na Waziri Mkuu mteule wa Hungary Magyar wajadili uhusiano wa mataifa mawili
Israel inaweza kuiangazia Uturuki kama adui baada ya Iran: Mwanadiplomasia mwandamizi wa Uturuki
Viongozi wa dunia wanakusanyika Uturuki katika Mkutano wa 5 wa Diplomasia wa Antalya
Uturuki yamshutumu Netanyahu kuhusu matamshi yake yanayomlenga Rais Erdogan
Erdogan, Macron wanajadili kuhusu mapatano ya Iran, Lebanon, Gaza
Uchimbaji mafuta wa Somalia: Rais Mohamud anaipongeza Uturuki kama mshirika 'anayetegemewa'
Shirika la ndege la Uturuki lapata Afisa Mtendaji Mkuu mpya
Meli ya Uturuki ya kuchimba mafuta baharini yawasili Somalia kwa operesheni ya kwanza nje ya nchi
“NATO inapaswa ‘kubadilika’ ili kukabiliana na changamoto za vita vya kisasa: Burhanettin Duran
Erdogan: Tumenuia kuwa kati ya nchi 10 bora kwenye mauzo ya zana za ulinzi
Uturuki yaadhimisha miaka 106 ya shirika la habari la Anadolu
Rais wa Uturuki atoa salamu za Pasaka kwa jamii ya Wakristo