| Swahili
UTURUKI
1 dk kusoma
Shirika la ndege la Uturuki lapata Afisa Mtendaji Mkuu mpya
Shirika hilo limemteua Murat Seker kama mwenyekiti wa bodi wa shirika hilo, huku Ahmet Olmustur akichukua nafasi ya Afisa Mtendaji Mkuu.
Shirika la ndege la Uturuki lapata Afisa Mtendaji Mkuu mpya
Shirika la ndege la Uturuki./Picha:@TurkishAirlines
tokea masaa 3

Murat Seker ameteuliwa kama mwenyekiti mpya wa bodi ya shirika hilo la ndege na kamati yake ya utendaji, wakati Ahmet Olmuştur alichaguliwa kama Afisa Mtendaji Mkuu wa shirika hilo.

Hatua hiyo inakuja baada kikao cha bodi ya shirika hilo la ndege kutangaziwa kuwa mwenyekiti aliye madarakani  Ahmet Bolat na Afisa Mtendaji Mkuu Bilal Eksi, wanastaafu.

Kabla ya uteuzi huo, Olmustur alikuwa akihudumu kam afisa mkuu wa biashara wa shirika hilo huku Murat Seker akishikilia nafasi ya Naibu Meneja Mkuu wa shirika la ndege la Uturuki, kuanzia mwaka 2016.