Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan na mwenzake wa Liberia, Joseph Nyuma Boakai, wamejadili uhusiano wa pande mbili na masuala ya kikanda wakati wa mazungumzo mjini Istanbul.
Viongozi hao wawili walikutana Ijumaa katika Banda la Vahdettin kabla ya kufanya majadiliano ya pande mbili.
Mkuu wa Mawasiliano wa Uturuki Burhanettin Duran na mshauri mkuu wa sera za kigeni na usalama wa Erdogan, Akif Cagatay Kilic, pia walihudhuria mazungumzo hayo na kiongozi huyo wa Afrika Magharibi.
Kulingana na taarifa kutoka kwa Kurugenzi ya Mawasiliano ya Uturuki, Erdogan alisema itakuwa "faida kwetu kuendelea kuchukua hatua za kutathmini uwezo wa kiasi cha biashara wa nchi hizo mbili."
Aliongeza kuwa Uturuki itafanya kazi ili kuimarisha ushirikiano na Liberia katika maeneo ikiwemo sekta ya ulinzi, usalama, elimu na usafiri.
Erdogan pia alimpongeza Boakai kwa kuchaguliwa kwa Liberia kama mwanachama asiye wa kudumu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
UTURUKI
1 dk kusoma
Rais Erdogan wa Uturuki na Rais Boakai wa Liberia wajadili uhusiano na masuala ya kikanda
Viongozi hao wawili walijadili uhusiano wa pande mbili, masuala ya kikanda na njia za kupanua ushirikiano, huku Rais wa Uturuki Erdogan akiipongeza Liberia kwa kuchaguliwa kwake katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

Soma zaidi


















