| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Uturuki inataka shule kufuta picha za wanafunzi zilizochapishwa mitandaoni bila idhini ya wazazi
Maelekezo haya yanakuja wakati ambapo, baadhi ya walimu nchini Uturuki wamekuwa na idadi kubwa ya wafuasi mitandaoni ikiwemo Instagram, TikTok na YouTube kwa kuweka maudhui ya wanafunzi wakiwa madarasani hivyo kuvutia idadi kubwa wa watu.
Uturuki inataka shule kufuta picha za wanafunzi zilizochapishwa mitandaoni bila idhini ya wazazi
Kijana akipiga picha akiwa na simu inayoonyesha nembo ya TikTok, mjini Bonn, Ujerumani, Februari 20, 2026.

Wizara ya Elimu ya Uturuki imezitaka shule zote nchini humo kuondoa picha na video za wanafunzi zinazochapishwa hadharani isipokuwa zile zilizoruhusiwa na wazazi, kama sehemu ya utekelezaji wa kanuni mpya yenye lengo la kuimarisha ulinzi wa taarifa binafsi.

Agizo hilo linataka shule kupitia upya mitandao yao na mitandao ya kijamii na kuondoa maudhui iliyochapishwa awali yenye picha za watoto au taarifa binafsi.

Wizara imesema hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya watakaokiuka kanuni hizo.

Wafanyakazi wa shule pia wametakiwa kukamilisha mafunzo ya lazima kuhusu ulinzi wa taarifa binafsi.

Maelekezo haya yanakuja wakati ambapo, baadhi ya walimu nchini Uturuki wamekuwa na idadi kubwa ya wafuasi mitandaoni ikiwemo Instagram, TikTok na YouTube kwa kuweka maudhui ya wanafunzi wakiwa madarasani hivyo kuvutia idadi kubwa wa watu.

Hatua hiyo, imeibua mjadala mpana mitandaoni kwamba inakiuka faragha ya wanafunzi.

Wasiwasi kama huo pia umeibuka kwengine. Nchini Hispania, walimu na wataalamu wa sheria wamekosoa ongezeko la wanaojiita “TeachTokers” kwa kutumia picha za wanafunzi wakiwa madarasani kwa kujinufaisha.

Agizo la Wizara ya Elimu ya Uturuki pia linakuja huku makampuni ya teknolojia yakiangaliwa kwa karibu kuhusu faragha ya mitandaoni.

Wiki iliyopita, Meta iliondoa kipengele kipya cha Instagram kinachotumia Akili Mnemba ambacho kinaruhusu watumiaji kupata picha kutoka kwenye akaunti za watu baada ya kukosolewa kwamba inaibua maswali ya faragha.

Kabla ya kuondolewa, watumiaji wa akaunti za wazi waliingizwa moja kwa moja, ikiwa na maana wengine wangetumia picha zilizopo na kuzibadilisha kwa kutumia Akili Mnemba bila taarifa ya ruhusu wa wamiliki.

Meta baadae ilikiri "kukosea" na kipengele hicho "hakipatikani tena."

Soma zaidi
Kuunga mkono Uturuki kufuatia jaribio la mapinduzi ilikuwa muhimu : Waziri wa zamani wa Uingereza
Erdogan: Uturuki itafanya kila iwezavyo kuzuia kutokea tena kwa mauaji ya kimbari kama ya Srebrenica
Uturuki na Misri zatia saini makubaliano ya kuweka msingi wa ushirikiano katika sekta ya ulinzi
Mawaziri wa Ulinzi wa Uturuki na Misri wakutana Ankara kuimarisha ushirikiano wa kiusalama
Manusura wa jaribio la mapinduzi la tarehe 15 Julai wakumbuka usiku wa upinzani miaka 10 baadaye
Uturuki yakumbuka miaka 10 ya jaribio la mapinduzi
Shirika la Ujasusi la Uturuki lamkamata gaidi mkuu wa Daesh katika operesheni ya Syria
Uturuki yasaidia waathirika wa tetemeko la ardhi Venezuela
Rais Erdogan aomboleza kifo cha aliyekuwa Amir wa Qatar
Erdogan wa Uturuki aadhimisha kumbukumbu ya mauaji ya kimbari ya Srebrenica
Uturuki inaadhimisha kumbukumbu ya miaka 31 ya mauaji ya halaiki ya Srebrenica
Sera na serikali ya Netanyahu ni 'mzigo' kwa Israel, eneo hilo na usalama wa kimataifa: Waziri Fidan
Rais Erdogan wa Uturuki na Rais Boakai wa Liberia wajadili uhusiano na masuala ya kikanda
Emine Erdogan ajadili masuala ya watoto, teknolojia na usalama na wenza wa viongozi wa NATO
Rais Erdogan: Mkutano wa NATO ulikuwa wa mafanikio makubwa
Trump ampongeza Rais Erdogan, akiuita mkutano wa NATO kuwa wa mafanikio
Uturuki yatafuta uhusiano wa kibiashara na uwekezaji zaidi na washirika wa NATO
Vikwazo vya CAATSA ni nini na kuondolewa kwake na Marekani kutainufaishaje Uturuki?
Rais Erdogan wa Uturuki aimarisha ahadi yake kwa NATO kupitia ufadili katika ulinzi
Viongozi wa NATO wafungua siku ya mwisho ya mkutano wa Ankara wakilenga Arctic, Iran, na Ukrain