| Swahili
UTURUKI
1 dk kusoma
Erdogan: Uturuki itafanya kila iwezavyo kuzuia kutokea tena kwa mauaji ya kimbari kama ya Srebrenica
Rais Recep Tayyip Erdogan amesema Uturuki itaendelea kuunga mkono amani na utulivu nchini Bosnia na Herzegovina, na kuutaja mkutano wa kilele wa NATO jijini Ankara kuwa mafanikio ya kidiplomasia.
Erdogan: Uturuki itafanya kila iwezavyo kuzuia kutokea tena kwa mauaji ya kimbari kama ya Srebrenica
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan akihutubia mkutano wa baraza la mawaziri katika Ikulu ya Rais mjini Ankara. / / AA

Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, amesema nchi yake itaendelea kufanya kila juhudi zinazohitajika kuhakikisha kuwa mauaji ya kimbari kama yale ya Srebrenica hayajirudii tena.

Akizungumza baada ya kuongoza kikao cha Baraza la Mawaziri jijini Ankara siku ya Jumatatu, Erdogan alisema Uturuki itaendelea kuunga mkono amani na utulivu nchini Bosnia na Herzegovina. Alisisitiza kuwa nchi yake itaendelea kujitahidi kuona Bosnia na Herzegovina inakuwa taifa lenye utulivu na ustawi, ambako watu wa dini, tamaduni na makabila mbalimbali wanaishi kwa amani na mshikamano.

Akizungumzia mkutano wa NATO uliofanyika Julai 7–8 katika mji mkuu wa Uturuki, Ankara, Erdogan alisema nchi yake imeongeza hadhi na ushawishi wake katika medani ya kimataifa kuliko wakati mwingine wowote kwa kufanikiwa kuwa mwenyeji wa mkutano huo wa kihistoria.

Alieleza kuwa mkutano huo ulikuwa miongoni mwa mikutano ya NATO iliyovutia ufuatiliaji mkubwa zaidi kutoka kwa vyombo vya habari ikilinganishwa na mikutano mingine aliyowahi kuhudhuria. Aidha, alisema mkutano huo umeonesha kwa kiwango kikubwa historia na utamaduni wa muda mrefu wa dola ya Uturuki.

Erdogan aliongeza kuwa katika kipindi ambacho "utaratibu wa zamani wa dunia uko katika hali mahututi, huku mfumo mpya ukiwa katika hatua za kuzaliwa," Ikulu ya Rais nchini Uturuki imekuwa kitovu muhimu cha diplomasia ya kimataifa.

CHANZO:AA