Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ametuma ujumbe wa rambirambi kwa Emir wa Qatar, Sheikh Tamim bin Hamad Al Thani, kufuatia kifo cha aliyekuwa kiongozi wa nchi hiyo 'Father Emir' (Emir Baba), Sheikh Hamad bin Khalifa Al Thani, aliyefariki dunia akiwa na umri wa miaka 74.
Katika ujumbe uliowekwa kwenye mitandao ya kijamii, Samia alitoa salamu za rambirambi kwa Emir, familia ya Al Thani na wananchi wa Qatar, akisema Tanzania inaungana na taifa hilo la Ghuba katika kipindi hiki cha maombolezo.
Sheikh Hamad aliongoza Qatar kuanzia mwaka 1995 hadi alipokabidhi madaraka kwa hiari yake kwa mwanawe mwaka 2013.
Anasifiwa sana kwa kuibadilisha Qatar na kuwa taifa kubwa duniani katika nyanja za nishati na diplomasia kupitia upanuzi wa sekta yake ya gesi asilia ya kumiminika (LNG) na kuanzishwa kwa kituo cha habari cha Al Jazeera.
‘‘Inna Lillahi wa inna ilayhi raji'un,’’ aliandika Rais Samia katika Ukurasa wake wa X, akiashiria msemo wa Waislamu kuwa ‘‘Sote tumetoka kwa Allah na sote tutarejea kwake.’’
Qatar imetangaza siku nne za maombolezo ya kitaifa kufuatia kifo chake.



















