| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Rais Erdogan aomboleza kifo cha aliyekuwa Amir wa Qatar
"Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kufariki kwa rafiki yangu mpendwa sana, Baba Emir wa Jimbo la Qatar, Sheikh Hamad bin Khalifa Al Thani," anasema Recep Tayyip Erdogan.
Rais Erdogan aomboleza kifo cha aliyekuwa Amir wa Qatar
Erdogan atoa rambi rambi kwa familia ya aliyekuwa Emir wa zamani wa Qatar Al Thani, / َAA

Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, siku ya Jumapili alitoa salamu za rambirambi kufuatia kifo cha aliyekuwa Amir wa Qatar, Sheikh Hamad bin Khalifa Al Thani, akiwa na umri wa miaka 74.

Katika ujumbe aliouchapisha kwenye akaunti yake ya mitandao ya kijamii, Erdogan alimwelezea Sheikh Hamad kama "rafiki wa karibu" na kusisitiza mchango wake katika kuimarisha uhusiano kati ya Uturuki na Qatar.

Rais Erdogan alisema kuwa alifanya kazi na Emir huyo wa zamani katika nyanja ya kimataifa wakati wa kipindi chake kama Waziri Mkuu, na alishuhudia binafsi juhudi zake za kukuza utulivu katika eneo hilo, amani katika ulimwengu wa Kiislamu, na ustawi wa watu wa Qatar.

"Nilipokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kufariki dunia kwa rafiki yangu mpendwa sana, 'Father Emir' (Emir Baba) wa Jimbo la Qatar, Sheikh Hamad bin Khalifa Al Thani," alisema Erdogan.

Rais huyo wa Uturuki alimpongeza Sheikh Hamad kwa mchango wake mkubwa katika kuendeleza uhusiano wa kisiasa, kibiashara, kijeshi, kiutamaduni na ule wa watu kwa watu kati ya nchi hizo mbili.

Erdogan aliombea dua kwa ajili ya marehemu Emir huyo wa zamani na kutoa rambirambi kwa kiongozi wa sasa wa Qatar, Sheikh Tamim bin Hamad Al Thani, pamoja na familia ya Al Thani, watu wa Qatar na ulimwengu mzima wa Kiislamu.

"Kwa niaba yangu binafsi, familia yangu na taifa langu, natoa rambirambi kwa ndugu yangu mpendwa, Emir wa Qatar Sheikh Tamim bin Hamad Al Thani, familia ya marehemu 'Father Emir', watu wa Qatar ambao ni marafiki na ndugu zetu, pamoja na ulimwengu wa Kiislamu," alisema.

Sheikh Hamad aliongoza Qatar kuanzia mwaka 1995 hadi 2013, alipokabidhi madaraka kwa mwanawe, Sheikh Tamim. Qatar ilitangaza kifo chake siku ya Jumapili.

CHANZO:َAA