| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Ghana yaonya raia wake kutosafiri Afrika Kusini kama hakuna ulazima
Wizara ya Mambo ya Nje ya Ghana inaeleza sababu kuwa vurugu za chuki zinazowalenga wahamiaji wa Kiafrika nchini Afrika Kusini, ikisema kuwa inazungumza na mamlaka na kufuatilia usalama wa raia wake.
Ghana yaonya raia wake kutosafiri Afrika Kusini kama hakuna ulazima
Mwezi uliopita Ghana iliwasafirisha mamia ya raia wake kutoka Afrika Kusini. / Reuters

Ghana imewataka raia wake kutosafiri kwenda Afrika Kusini kama hakuna ulazima wa kufanya hivyo hadi pale watakapofahamishwa kuhusu maelekezo mengine kutokana na kukithiri kwa mashambulizi ya chuki yanayolenga wahamiaji wa Kiafrika.

Katika taarifa, Wizara ya Mambo ya Nje ya Ghana ilisema Jumatatu kuwa makundi yanayojiita kuwa ya vuguvugu dhidi ya wahamiaji Afrika Kusini yamekuwa yakifanya mashambulizi dhidi ya raia wa kigeni wa Afrika, kusababisha majeraha, kupora, biashara kufungwa na mali kupotea.

Wizara imetoa wito kwa raia wa Ghana kuwa makini zaidi katika mipango yao ya safari na kusafiri tu pale palipo na ulazima wa kwenda Afrika Kusini hadi pale hali ya usalama itakapokuwa shwari.

Raia wa Ghana wanaoishi Afrika Kusini wameshauriwa kuwasiliana mara kwa mara na Ubalozi wa Ghana kupata taarifa za usalama na msaada kutoka kwa ubalozi.

Juhudi za kidiplomasia

Wizara inasema serikali ya Ghana imeanzisha juhudi za kidiplomasia na mamlaka za Afrika Kusini kuhusu matukio hayo.

Iliongeza kuwa balozi mdogo wa Afrika Kusini nchini Ghana ameitwa na Wizara ya Mambo ya Nje kutoa ufafanuzi, suala hilo limefikishwa kwa Umoja wa Afrika, na juhudi zinaendelea kusaidia raia wa Ghana na kuwasafirisha iwapo kuna ulazima wa kufanya hivyo.

Ghana pia ilitoa wito kwa serikali ya Afrika Kusini kuhakikisha usalama wa raia wa Afrika wanaoishi nchini humo na kuhakikisha hali ya usalama inarudi kama kawaida.

Vurugu dhidi ya wahamiaji zimeripotiwa katika baadhi ya maeneo nchini Afrika Kusini tangu Aprili, huku biashara zinazomilikiwa na wahamiaji zikishambuliwa na watu kadhaa kujeruhiwa na raia wengine wa kigeni kuondolewa katika maeneo yaliyoathiriwa.

Mwezi uliopita, Ghana iliomba suala hilo lijadiliwe rasmi katika Mkutano wa 8 wa katikati ya mwaka wa Umoja wa Afrika uliopangwa kufanyika El-Alamein nchini Misri kuanzia Juni 24-27.

Soma zaidi
Maambukizi ya Ebola DRC yaongezeka hadi 282, serikali imesema
Mahakama ya usuluhishi yakataa madai ya Dola milioni 134 ya Rwanda kwa mkataba wa Uingereza
Mamia waandamana nje ya kituo cha karantini cha Ebola cha Kenya kwa raia wa Marekani
Maombolezi yaendelea kwa wanafunzi 16 waliokufa moto shuleni Kenya huku lawama zikienea
Wapiga kura wajitokeza kwa wingi katika Uchaguzi Mkuu nchini Ethiopia
Wagonjwa watano wapona Ebola nchini DRC, WHO yathibitisha
Mkuu wa WHO ahimiza mazishi salama huku mlipuko wa Ebola DRC ukiendelea kukua
Mlipuko wa Ebola katika DRC unazidi juhudi za kukabiliana na ugonjwa huo : MSF
RSF ya Sudan yaua raia 27 katika mashambulizi dhidi ya vijiji vya Kordofan Kaskazini
Zambia yathibitisha hakuna maambukizi ya Ebola kwa walioshukiwa kuvuka mpaka
Marekani bado yakazia macho kituo cha Ebola kilichopendekezwa nchini Kenya
Marekani yatuma vifaa vya kijeshi vya thamani ya $2.3M kwa Niger licha ya uhusiano mgumu
Saudi Arabia yatangaza kumalizika kwa ibada ya Hajj huku  mahujaji wakifika milioni 1.7 mwaka 2026
Familia ya aliyekuwa Rais wa Zambia Lungu yaelekea Mahakama ya Rufani kutokana na mzozo na serikali
Wanafunzi 8 nchini Kenya washikiliwa na polisi kufuatia ajali ya moto katika shule ya wasichana
WHO yatangaza mgonjwa wa kwanza kupona mlipuko wa Ebola DRC
Maafisa wa uhamiaji Marekani washtumiwa kwa kumtesa raia wa Ghana aliyekuwa mjamzito
Mahakama ya Kenya yasitisha kwa muda mpango wa kituo cha karantini cha Marekani nchini humo
Kituo cha Afya Afrika kinalenga kupata chanjo ya Ebola kufikia mwishoni mwa 2026
Kenya yaidhinisha kituo cha Marekani kwa karantini ya Ebola kutokana na mlipuko DRC, afisa asema