| Swahili
ULIMWENGU
1 dk kusoma
Iran: Hatuna mazungumzo yoyote na Marekani
Iran imekuwa na udhibiti wa njia hiyo toka kuanza kwa vita vya Mashariki ya Kati, Februari 28.
Iran: Hatuna mazungumzo yoyote na Marekani
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Esmaeil Baqaei amesema kuwa taifa hilo halijafanya mazungumzo yoyote na Marekani kuhusu mustakabali wa Mlango Bahari

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Esmaeil Baqaei  amesema kuwa taifa hilo halijafanya mazungumzo yoyote na Marekani kuhusu mustakabali wa Mlango Bahari wa Hormuz.

"Hatuna mazungumzo yoyote na Marekani, isipokuwa tuna mazungumzo na Oman kuhusu Oman kwa ajili ya Mlango Bahari wa Hormuz,” alisema waziri huyo.

Iran imekuwa na udhibiti wa njia hiyo toka kuanza kwa vita vya Mashariki ya Kati, Februari 28, mwaka huu.

Wakati huo huo, Iran imesisitiza kuwa njia hiyo itaendelea kurahisisha usafirishwaji wa nishati mbalimbali, kwa kupata kibali kutoka Iran.

Akizungumzia mazungumzo na Oman, Baqaei alisema kuwa, yanaridhisha, yakiwa na lengo la kuzindua njia mpya ya kupitia.

"Ni matumaini yetu kuwa, wenzetu watakubaliana na mpango huu,” alieleza.

 

 

CHANZO:AFP