| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Libya: Wahamiaji 17 wamekufa maji, wengine 9 hawajulikani walipo
Takriban wahamiaji 17 wamekufa maji na wengine tisa hawajulikani walipo baada ya boti yao kuharibika na kuelea kwa siku nane katika Bahari ya Mediterania, Shirika la Msalaba Mwekundu la Libya na vyanzo vya usalama vya Libya vilisema Jumatano.
Libya: Wahamiaji 17 wamekufa maji, wengine 9 hawajulikani walipo
Libya ni njia wanayotumia wahamiaji, wengi wao wakitoka Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, kukimbilia Ulaya. / Reuters

Shirika la Msalaba Mwekundu lilisema katika taarifa kwamba wafanyakazi wake wa kujitolea kwa kushirikiana na vikosi vya majini na walinzi wa pwani wa Jeshi la Kitaifa la Libya waliwaokoa manusura saba katika operesheni ya uokoaji iliyofanyika karibu na mji wa Tobruk mashariki mwa Libya, karibu na mpaka wa Misri.

Libya ni njia wanayotumia wahamiaji, wengi wao wakitoka Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, kuhatarisha maisha yao kukimbilia Ulaya kupitia jangwa na bahari wakitafuta kuepuka migogoro na umaskini.

Vyanzo vya usalama vilisema vinakadiria miili ya wahamiaji tisa waliopotea kusombwa na maji hadi kufika ufukweni katika siku chache zijazo.

Picha zilizowekwa mtandaoni na Shirikia la Msalaba Mwekundu zilionyesha wafanyakazi waliojitolea wakiweka miili hiyo kwenye mifuko ya plastiki nyeusi na kuipakia kwenye nyuma ya magari madogo ya kubeba mizigo.

Jumanne, mwanasheria mkuu wa nchi alisema Mahakama ya Jinai ya Tripoli iliwahukumu wanachama wanne wa “kundi la kihalifu” huko Zuwara, magharibi mwa Libya, hadi kifungo cha miaka 22 jela kwa biashara ya usafirishaji haramu wa binadamu, utekaji nyara kwa ajili ya fidia, na mateso.

Katika kesi nyingine, Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Umma iliamuru Jumatatu kukamatwa kwa genge jingine linalodaiwa kuwasafirisha wahamiaji kutoka Tobruk kwa kutumia boti chakavu, na kusababisha vifo vya raia 38 wa Sudan, Misri na Ethiopia, kwa mujibu wa mwanasheria mkuu.

CHANZO:Reuters