| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Nigeria yawapata magaidi wanne na hatia kwa mauaji ya kanisani mwaka 2022
Jaji nchini Nigeria amewapata na hatia wanaume wanne katika kesi ya ugaidi kuhusu mauaji katika kanisa 2022.
Nigeria yawapata magaidi wanne na hatia kwa mauaji ya kanisani mwaka 2022
Mahakama nchini Nigeria Juni 3, 2026 imewahukumu wanaume wanne kuuawa kutokana na mauaji ya mwaka 2022 katika kanisa. / Reuters

Jaji nchini Nigeria siku ya Jumatano amewapata na hatia wanaume wanne katika kesi ya ugaidi kuhusu mauaji katika kanisa 2022, huku akimuacha huru mtu wa tano.

Kufyatua risasi na kurusha mabomu katika kanisa la Katoliki la St Francis Xavier mji wa Owo, kusini magharibi mwa jimbo la Ondo, kulisababisha vifo vya zaidi ya watu 40 na wengine 100 kujeruhiwa, kulingana na mwendesha mashtaka.

Jaji Emeka Nwite wa Mahakama Kuu ya Abuja iliwapata na hatia Idris Abdulmalik Omeiza, Al Qasim Idris, Jamiu Abdulmalik na Abdulhaleem Idris ya makosa tisa yaliyowasilishwa chini ya Sheria ya Ugaidi ya 2022 (Kuzuia na Kupinga), ikiwa ni pamoja na kujiunga na kundi la kigaidi hadi kupanga njama na kufanya mauaji.

Walihukumiwa kifungo cha maisha kila mmoja, na kuuawa, ingawa kwa sheria ya Nigeria watu hawauawi.

'Haki imetendeka'

Mshtakiwa wa tano, Momoh Otuho Abubakar, hakupatikana na hatia na kuachiwa huru.

"Haki imetendeka, haki imepatikana kwa waliouawa kikatili," mwendesha mashtaka Ayodeji Adedipe aliwaambia waandishi wa habari.

Wakili wa upande wa washtakiwa Abdullahi Muhammad amesema watakata rufaa ya hukumu hiyo.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Marekani yawawekea vikwazo makamanda wanaohusishwa na vita mashariki mwa DRC
Uwanja wa ndege wa DRC katika eneo lilokumbwa na mlipuko wa Ebola wafunguliwa tena
Ghana yaonya raia wake kutosafiri Afrika Kusini kama hakuna ulazima
Wanafunzi tisa wafikishwa mahakamani Kenya kwa madai ya kuchoma moto shule
Serikali ya Tanzania inataka utatuzi wa haraka wa kero za watumishi wa umma
Rais Faye wa Senegal aunda serikali mpya bila chama cha Sonko
Mahakama Kuu Kenya yaendelea kuzuia mpango wa kujenga kituo cha Ebola
Maambukizi ya Ebola DRC yaongezeka hadi 282, serikali imesema
Mahakama ya usuluhishi yakataa madai ya Dola milioni 134 ya Rwanda kwa mkataba wa Uingereza
Mamia waandamana nje ya kituo cha karantini cha Ebola cha Kenya kwa raia wa Marekani
Maombolezi yaendelea kwa wanafunzi 16 waliokufa moto shuleni Kenya huku lawama zikienea
Wapiga kura wajitokeza kwa wingi katika Uchaguzi Mkuu nchini Ethiopia
Wagonjwa watano wapona Ebola nchini DRC, WHO yathibitisha
Mkuu wa WHO ahimiza mazishi salama huku mlipuko wa Ebola DRC ukiendelea kukua
Mlipuko wa Ebola katika DRC unazidi juhudi za kukabiliana na ugonjwa huo : MSF
RSF ya Sudan yaua raia 27 katika mashambulizi dhidi ya vijiji vya Kordofan Kaskazini
Zambia yathibitisha hakuna maambukizi ya Ebola kwa walioshukiwa kuvuka mpaka
Marekani bado yakazia macho kituo cha Ebola kilichopendekezwa nchini Kenya
Marekani yatuma vifaa vya kijeshi vya thamani ya $2.3M kwa Niger licha ya uhusiano mgumu
Saudi Arabia yatangaza kumalizika kwa ibada ya Hajj huku  mahujaji wakifika milioni 1.7 mwaka 2026