| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Usambazaji wa gesi wa Uturuki, Azerbaijan nchini Syria kutasaidia maendeleo, usalama: Rais Erdogan
Kuna fursa kubwa za kuimarisha ushirikiano kwa kusambaza gesi kutoka kwa mataifa yanayozungumza Kituruki kupitia Azerbaijan na Uturuki, anasema Rais wa Uturuki.
Usambazaji wa gesi wa Uturuki, Azerbaijan nchini Syria kutasaidia maendeleo, usalama: Rais Erdogan
Rais Erdogan akizungumza katika Kongamano Ukumbi wa Mkutano wa Lutfi Kirdar jijini Istanbul, Uturuki, Mei 22, 2026. / Anadolu Agency

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amesema Jumatatu kuwa usambazaji wa gesi kwenda Syria ulioanzishwa kupitia mpango wa Uturuki na Azerbaijan utasaidia maendeleo ya nchi na usalama katika kanda.

“Mchango wa usambazaji wa gesi nchini Syria, ambao ulianza mwezi Agosti kutokana na mpango wa Uturuki na Azerbaijan, kwa maendeleo ya nchi hizi na usalama katika kanda haupingiki,” Erdogan amesema kupitia ujumbe katika ufunguzi wa Wiki ya Nishati ya Baku.

Erdogan anasema yaliyojiri hivi karibuni kwa mara nyingine yameonesha umuhimu wa hatua zilizochukuliwa pamoja na Azerbaijan katika masuala ya nishati, na nchi hizo mbili zimekuwa na miradi mikubwa ambayo awali yalionekana kama hayawezekani.

Alieleza kuhusu miradi ya gesi asilia ya Baku-Tbilisi-Ceyhan, Baku-Tbilisi-Erzurum na Trans-Anatolia, ambayo ilianzishwa na Azerbaijan na kukamilishwa kwa mchango wa Georgia.

Uhusiano kati ya Uturuki na Azerbaijan umeimarika zaidi kupitia ushirikiano wa Azeri-Chirag-Gunashli na Shah Deniz, ilihali ushirikiano mpya wa Shafag-Asiman unaonesha ushirikiano wa nishati wa mataifa mawili unaendelea bila kusita, aliongeza.

Erdogan anasema bomba la gesi la Igdir-Nakhchivan, ambalo lilianza kutumika mwaka uliopita, limeimarisha upatikanaji wa bidhaa hiyo katika eneo la Nakhchivan nchini Azerbaijan.

Kuunganisha umeme kati ya Uturuki na Azerbaijan bado ni muhimu kimkakati, alisema, akiongeza kuwa Mradi wa Usambazaji Umeme na ule wa Biashara kati ya Uturuki, Azerbaijan, Georgia na Bulgaria unatarajiwa kuchangia katika upatikanaji wa nishati kwenye kanda nzima.

Kuhusu usambazaji wa nishati katika kanda, Erdogan anasema kuwa kuna fursa za kuimarisha ushirikiano kwa kuuza gesi kutoka mataifa yanayozungumza Kituruki kupitia Azerbaijan na Uturuki.

Aliongeza kuwa bomba la Baku-Tbilisi-Ceyhan linatumiwa zaidi kusafirisha raslimali asilia za Kazakhstan hadi katika soko la mataifa ya Magharibi.

Uturuki ina dira ya kuhakikisha uthabiti kote katika masuala ya nishati, ikiwemo nishati endelevu na safi, kulingana na uhakika na kuzingatia mazingira, Erdogan anasema.

Uturuki, aliongeza, itaimarisha dhamira yake ya kuwa miongoni mwa nchi za kupigiwa mfano kwa kuwa wenyeji wa kongamano la COP31 jijini Antalya Novemba 9-20.

CHANZO:Anadolu Agency
Soma zaidi
Erdogan aadhimisha Eid al-Adha na ujumbe wa mshikamano wa Gaza, amkemea 'mnyanyasaji' Netanyahu
Erdogan aadhimisha Eid al-Adha kwa ujumbe wa umoja Gaza, amkashifu "muuaji" Netanyahu
Israel inaendelea na uvamizi na mauaji Gaza na Lebanon licha ya makubaliano ya kusitisha mapigano
Uturuki na nchi nyengine 7 zalaani udhalilishaji wa Israel dhidi ya wanaharakati wa Flotilla
Wataalamu wanakusanyika katika Jukwaa la Afrika 2026 ili kujadili uhusiano kati ya Uturuki na Afrika
Idara ya Ujasusi ya Uturuki yanasa washukiwa 10 wa Daesh katika operesheni ya Syria
Uturuki imekuwa kitovu cha nishati, mtetezi wa amani huku kukiwa na mvutano wa kikanda: Rais Erdogan
Erdogan wa Uturuki asisitiza kuunga mkono uhuru wa Sudan katika mazungumzo na Waziri Mkuu Idris
Rais Erdogan wa Uturuki amlaki Waziri Mkuu wa Sudan jijini Ankara
Rais Erdogan amwambia von der Leyen kuwa mvutano wa kikanda unahitaji uhusiano wa Uturuki na EU
Waturuki walio diaspora ni muhimu kwa ushawishi unaokua wa Uturuki duniani, anasema balozi
Uchokozi' wa Israel lazima ukomeshwe kwa amani ya Mashariki ya Kati: Rais wa Uturuki Erdogan
Erdogan atoa wito wa ushirikiano kati ya nchi za Turkic katika ulinzi, AI na usalama wa mtandao
Marais wa Uturuki na Uzbekistan wajadili ushirikiano wa ulinzi na biashara mjini Turkistan
Rais Erdogan, aisifia Ukanda wa Kati kuwa ‘Barabara ya Silki ya kisasa’ katika ziara yake Kazakhstan
Rais wa Uturuki apewa mapokezi makubwa Kazakhstan
Uturuki yapinga madai “yasiyo na msingi kabisa” ya kuingilia siasa za Somalia
Rais wa Uturuki aelekea Kazakhstan kuhudhuria mkutano wa viongozi wa nchi za Turkic
Uturuki yakana madai ya kuingilia siasa za ndani za Somalia
Uturuki iko tayari kuanzisha mazungumzo ya moja kwa moja na Armenia: afisa