Chama tawala cha Guinea kilishinda kwa kishindo katika uchaguzi wa wabunge na mitaa, baraza la uchaguzi lilisema Ijumaa.
Uchaguzi wa Jumapili iliyopita ulikuwa hatua ya kurejea katika utawala wa kidemokrasia baada ya mapinduzi ya mwaka 2021 katika nchi hiyo ya Afrika Magharibi.
Vuguvugu la Rais Mamady Doumbouya la Kizazi cha Kisasa na Maendeleo lilipata wingi wa viti 147 katika Bunge la Kitaifa na pia katika mabaraza ya manispaa, kulingana na matokeo ya muda yaliyotangazwa na Kurugenzi Kuu ya Uchaguzi.
Mahakama ya juu zaidi itatangaza matokeo ya mwisho katika muda wa wiki mbili.
Doumbouya alichaguliwa kuwa rais kwa muhula wa miaka saba mwezi Disemba.
ZILIZOPENDEKEZWA
CHANZO:AFP



















