Kiungo wa timu ya taifa ya Colombia, Jáminton Campaz anadaiwa kujificha, yeye pamoja na familia yake, akihofia usalama wake baada ya timu hiyo kuondolewa kwenye michuano ya Kombe la Dunia mwaka huu.
Campaz anadaiwa kuigharimu timu yake, baada ya kushindwa kufunga bao muhimu, wakati wa mechi dhidi ya Uswisi, kabla ya Colombia kutolewa kwa mikwaju ya penati.
Tukio hilo, limeibua kumbukumbu ya miaka 32 iliyopita, wakati wa michuano ya Kombe la Dunia nchini Marekani, ambako aliyekuwa beki wa timu ya taifa ya Colombia, Andrés Escobar, alipigwa risasi na kufa, siku chache baada ya kujifunga goli dhidi ya wenyeji Marekani, na hivyo kuifanya Colombia itolewe kwenye michuano hiyo.
Hali hiyo, pia imemkumba mshambuliaji wa Norway, Alexander Sorloth ambaye anaendelea kupokea vitisho mitandaoni, akituhumiwa kwa kushindwa kumpa pasi muhimu, Erling Haaland, ambaye alikuwa katika nafasi nzuri ya kufunga dhidi ya Uingereza.


Tazama Video zaidi
Soka laweka maisha yake rehani
Kiungo wa timu ya taifa ya Colombia, Jáminton Campaz anadaiwa kujificha, yeye pamoja na familia yake, akihofia usalama wake baada ya timu hiyo kuondolewa kwenye michuano ya Kombe la Dunia mwaka huu.
Tazama Video zaidi