Mohamed Salah aliisaidia Misri kupata ushindi wake wa kwanza katika Kombe la Dunia walipojiimarisha na kuifunga New Zealand 3-1 siku ya Jumapili, kuwafanya kuongoza Kundi G pamoja na kuwapa matumaini ya kufika hatua ya mtoano.
Misri, ambao ni miongoni mwa timu inayopewa nafasi ya kufika mbali ikiwa na Salah na Omar Marmoush katika eneo la mashambulizi, walikuwa na mashaiki wa kutosha katika uwanja wa BC Place.
Hata hivyo, kushindwa kuwa makini kwenye ulinzi kuliwaponza na mchezaji wa safu ya ulinzi wa New Zealand Finn Surman akaipatia timu yake goli katika dakika ya 15 kutokana na kona ya Tim Payne.
Mostafa Ziko alifunga bao la kusawazisha katika dakika ya 58. Dakika tisa baadaye nahodha Salah akaongeza goli la pili na Mahmoud Trezeguet kukamilisha karamu ya magoli matatu kwa Mafarao.
Misri, ambayo ilitoka sare ya 1-1 na Ubelgiji katika mechi yao ya kwanza, sasa inaongoza kundi hilo ikiwa na alama nne baada ya mechi mbili. Katika mechi yao kwanza, New Zealand ilitoka sare ya 2-2 na Iran katika mechi yao ya kwanza, na wako chini ya masimamo kwenye kundi ikiwa na alama moja.














