| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Mshikamano uliotibua jaribio la mapinduzi unapaswa kuongoza vizazi vijavyo: Waziri wa Ulinzi
Yasar Guler anasema kuwa mustakabali wa nchi unategemea kuendelea kwa moyo uliojitokeza wakati wa jaribio la mapinduzi lililoshindwa, pamoja na kudumisha mshikamano wa kitaifa dhidi ya vitisho vya kijeshi na vinavyotumia mbinu mbalimbali.
Mshikamano uliotibua jaribio la mapinduzi unapaswa kuongoza vizazi vijavyo: Waziri wa Ulinzi
Waziri wa ulinzi wa Uturuki asema mshikamano uliotibua jaribio la mapinduzi unapaswa kuongoza vizazi vijavyo. / / Reuters

Waziri wa Ulinzi wa Uturuki, Yasar Guler, amesema kuwa jukumu la taifa si tu kukumbuka jaribio la mapinduzi lililoshindwa la Julai 15, 2016, bali pia kuhifadhi mafunzo na moyo uliodhihirishwa siku hiyo na kuurithisha kwa vizazi vijavyo.

Akizungumza Jumanne katika makao makuu ya Wizara ya Ulinzi jijini Ankara wakati wa maadhimisho ya Siku ya Demokrasia na Umoja wa Kitaifa, alisema jaribio hilo lililenga kuvuruga utaratibu wa kidemokrasia wa Uturuki, mapenzi ya wananchi na uhuru wa taifa, lakini lilizimwa kutokana na mshikamano wa wananchi pamoja na vikosi vya usalama chini ya uongozi wa Rais Recep Tayyip Erdogan.

“Jukumu letu la kweli ni kuendeleza moyo wa mshikamano tuliyokabidhiwa usiku huo na kuhakikisha inawafikia vizazi vijavyo bila kupoteza thamani yake,” alisema Guler.

Waziri huyo pia alisema mpango wa “Uturuki Isiyo na Ugaidi” haupaswi kutazamwa kama sera ya kiusalama pekee, bali kama dira ya kitaifa inayolenga kuimarisha umoja, kumaliza ugaidi na kuhakikisha amani na ustawi wa kudumu.

Aliongeza kuwa mataifa kwa sasa hayakabiliwi tena na vitisho vya kijeshi pekee, bali pia na ugaidi, mashambulizi ya mtandaoni, kampeni za upotoshaji wa taarifa, shinikizo za kiuchumi na juhudi za kuchochea migawanyiko ya kijamii.

Kwa mujibu wa Guler, umoja wa kitaifa ndio ngao muhimu zaidi ya Uturuki dhidi ya vitisho vya aina zote.

Akizungumzia operesheni zinazoendelea za Jeshi la Uturuki, alisema jeshi hilo limeimarika zaidi na kuongeza uwezo wake wa kiutendaji baada ya kuwaondoa wanachama wa Shirika la Kigaidi la Fetullah (FETO) kutoka ndani ya taasisi hiyo.

CHANZO:AA