Fenerbahce imeifunga Lyon 2-1 siku ya Jumatano na kufanikiwa kuingia hatua ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa mara ya kwanza tangu kufika hatua ya makundi msimu wa 2008-09.
Timu hiyo ya Uturuki ilivuka hatua nyingine kwa ushindi wa jumla ya magoli 3-2 baada ya kutoka sare 1-1 katika mechi ya mkondo wa kwanza jijini Istanbul, na kurejea katika mashindano ya Ulaya.
Fenerbahce hawakuruhusiwa na Shirikisho la Soka Ulaya (UEFA) kushiriki misimu miwili ya Ligi hiyo kufuatia uchunguzi wa kupanga mechi 2011, jambo lililoifanya timu hiyo ya Uturuki kutoshiriki mashindano ya Ulaya licha ya kushinda taji la Ligi Kuu ya Uturuki 2010-11 Super Lig.
Baadaye klabu hiyo na rais wake wa zamani Aziz Yildirim waliondolewa lawama, huku upande wa mashtaka 2016 ukieleza kesi hiyo ya kupanga mechi ilikuwa njama ya wanachama wa Kundi la Kigaidi la Fetullah (FETO) ambao walikuwa wameingilia idara ya mahakama ya Uturuki na polisi.
Katika mechi hiyo ya Jumatano Lyon walijitahidi kupunguza tofauti ya magoli katika dakika 35 ya mchezo, lakini Fenerbahce wakafanikiwa kuondoa hatari.
Timu hiyo ya Uturuki ilifanikiwa kupata ushindi 2-1, na kukamilisha matokeo jumla kuwa 3-2 ikiwa yanatosha kuwapa nafasi katika Ligi ya Mabingwa barani Ulaya.

















