| Swahili
MICHEZO
1 dk kusoma
Mkuu wa shirikisho la Afrika aunga mkono Tanzania, Kenya na Uganda kuandaa AFCON 2027
Rais wa CAF Patrice Motsepe amekiri kuwepo kwa changamoto wakati wa maandalizi lakini akasema CAF imedhamiria kusaidia mataifa hayo matatu kukamilisha yanayohitajika kwa wakati ufaao.
Mkuu wa shirikisho la Afrika aunga mkono Tanzania, Kenya na Uganda kuandaa AFCON 2027
Rais wa CAF Patrice Motsepe yuko kwenye ziara ya siku mbili nchini Tanzania na Kenya kukagua hatua za maandalizi. Picha / CAF

Patrice Motsepe, rais wa Shirikisho la Soka baranI Afrika (CAF), anasema bado ana matumaini kuwa Kenya, Tanzania na Uganda watafanikisha uwenyeji wa AFCON 2027, akipuuzia uvumi kuwa mashindano hayo yanaweza kupelekwa sehemu nyingine.

Motsepe alikiri kuwepo kwa changamoto wakati wa maandalizi lakini akasema CAF imedhamiria kusaidia mataifa hayo matatu kukamilisha yanayohitajika kwa wakati ufaao.

"Lazima kuwe na changamoto na maeneo ambayo yanahitaji kuimarishwa, lakini tunatakiwa kujiamini kama Afrika Mashariki na Waafrika kuwa tutafanya kazi pamoja na kukamilisha kinachohitajika kwa wakati muafaka," aliwaambia waandishi wa habari siku ya Alhamisi.

Hata hivyo, Motsepe alikiri kuwa, kazi zaidi inahitajika kufanywa, huku nchi hizo tatu zikijitahidi kukamilisha ukarabati na ujenzi wa miundombinu kabla ya mashindano hayo.

"Nafurahia kazi nzuri inayoendelea nchini Tanzania. Na, imebaki miezi tisa na baadhi ya msisitizo wangu ni kuharakisha kazi hiyo, na tuko hapa kushirikiana, kutoa msaada. Hii ni AFCON yetu."

Michuano ya 2027, ni ya kwanza kuwa na mwenyeji zaidi ya mmoja ambapo Kenya, Tanzania na Uganda, wanatarajiwa kuwa wenyeji kwa mashindano yatakayoanza Juni 19 hadi Julai 17.

CHANZO:TRT Afrika Swahili