| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Fidan wa Uturuki na Gil wa Venezuela wajadili msaada kwa mitetemeko iliyosababisha vifo zaidi ya 200
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan amezungumza na mwenzake wa Venezuela Yvan Gil kumpa salamu za rambirambi na kujadili misaada, vyanzo vimeiambia AA.
Fidan wa Uturuki na Gil wa Venezuela wajadili msaada kwa mitetemeko iliyosababisha vifo zaidi ya 200
Mitetemeko ya kiwango cha 7.2 na 7.5 imeikumba Venezuela Jumatano, kusababisha uharibifu mkubwa. / AP

Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan amefanya mazungumzo kwa njia ya simu na mwenzake wa Venezuela Yvan Gil kujadili janga la tetemeko la ardhi na mahitaji ya misaada, vyanzo vya kidiplomasia vya Uturuki vimeiambia Anadolu Agency.

Wakati wa mazungumzo hayo siku ya Alhamisi, Fidan alipata taarifa kutoka kwa Gil kuhusu athari za mitetemeko na mahitaji ya misaada.

Akituma salamu zake za rambirambi kwa niaba ya watu wa Uturuki, Fidan anasema Uturuki itaendelea kutoa misaada, kulingana na vyanzo hivyo.

Mitetemeko hiyo miwili iliikumba Venezuela Jumatano, ikiwa na kiwango cha 7.2 huko San Felipe kaskazini magharibi mwa Venezuela, ikifuatiwa na kiwango cha 7.5 kusini mashariki mwa Yumare.

Jorge Rodriguez, rais wa Bunge, anasema kumekuwa na mitetemeko midogo 138 tangu kutokea kwa janga hilo.

Rodriguez anasema idadi ya waliofariki imeongezeka hadi 188, huku watu 1520 wakijeruhiwa, 200 wamekwama kwenye vifusi na wengine 157 hawajulikani waliko kutokana na janga hilo.

Amesema miundombinu 346 iliharibiwa, ikiwemo majengo 250 maeneo 20 ya maduka, mengi yao yakiwa katika jimbo la La Guaira. Huduma katika hospitali nane pia zilitatizwa, kulazimisha mamlaka kuwapeleka wagonjwa katika hospitali zingine.

Kaimu Rais Delcy Rodriguez ametangaza maombolezi ya kitaifa kufuatia janga hilo.

Serikali ya Venezuela pia imetangaza mfuko maalum wa dola milioni 200 kwa ajili ya juhudi za haraka za ujenzi, ikiwemo ujenzi wa nyumba zilizoharibiwa na hospitali.

CHANZO:aa