| Swahili
UTURUKI
1 dk kusoma
Erdogan wa Uturuki na Merz wa Ujerumani wazungumza kwa simu kuhusu masuala ya kimataifa
Uturuki inatarajia kuona "dhamira thabiti" katika mkutano wa NATO utakaofanyika Ankara, katika kuimarisha ulinzi wa Ulaya na kudumisha "mshikamano wa Kanda ya Marekani Kaskazini na Ulaya"
Erdogan wa Uturuki na Merz wa Ujerumani wazungumza kwa simu kuhusu masuala ya kimataifa
Rais Recep Tayyip Erdogan akimpokea Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz katika Ikulu ya Rais mnamo tarehe 30 Oktoba 2025. / / AA Archive

Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, na Kansela wa Ujerumani, Friedrich Merz, wamezungumza kwa njia ya simu kuhusu masuala ya kikanda na kimataifa pamoja na uhusiano wa mataifa hayo mawili, kwa mujibu wa Kurugenzi ya Mawasiliano ya Uturuki.

Katika mazungumzo hayo, Rais Erdogan alisema kuwa Uturuki inalenga kuimarisha zaidi uhusiano wake na Ujerumani, akisisitiza umuhimu wa pande zote mbili kuendelea kuchukua hatua za pamoja ili kufanikisha lengo hilo.

Erdogan pia alisema kuwa Uturuki inatarajia kuona "dhamira thabiti" katika mkutano wa NATO utakaofanyika Ankara, katika kuimarisha ulinzi wa Ulaya na kudumisha "mshikamano wa Kanda ya Marekani Kaskazini na Ulaya" kati ya washirika wa NATO.

Kuhusu vita vinavyoendelea kati ya Urusi na Ukraine, Erdogan alisema kuwa Uturuki inaendelea kufanya juhudi za kufanikisha amani ya kudumu na kurejesha mazungumzo ya kidiplomasia kati ya pande husika.

CHANZO:Anadolu Agency