Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan amesema mashambulizi ya Israel ni miongoni mwa vitisho vikubwa kwa usalama wa Syria, akishtumu serikali ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu kwa kuchochea vurugu kote katika kanda.
Akizungumza pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria Asaad Hassan al Shaibani baada ya mkutano jijini Ankara siku ya Alhamisi, Fidan anasema mashambulizi ya Israel yanatatiza uhuru wa mipaka ya Syria.
"Mashambulizi ya Israel yanayolenga uhuru wa mipaka ya Syria ni miongoni mwa vitisho vikubwa vya usalama wa nchi hiyo," alisema.
Akizungumzia kuhusu mpango wa amani wa Gaza, Fidan anasema mashambulizi ya Israel yanayoendelea yanaonesha kuwa "Netanyahu hataki amani."
"Tunaona serikali ya Netanyahu imezidisha mashambulizi yake ya kigaidi Ukingo wa Magharibi na mji wa Jerusalem," aliongeza.




















