| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Wanajeshi wa Uganda na Congo wawaokoa mateka 200 kutoka kwa magaidi wa ADF
Wanajeshi wa Uganda na Congo waliwaokoa takriban raia 200 katika uvamizi dhidi ya kambi ya magaidi mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wiki iliyopita, jeshi la Uganda lilisema Jumatatu.
Wanajeshi wa Uganda na Congo wawaokoa mateka 200 kutoka kwa magaidi wa ADF
Wanajeshi wa Uganda na Kongo wamewaokoa watu 200 waliotekwa nyara kutoka kwa magaidi wa ADF. /AP / AP
tokea masaa 2

Wanajeshi wa Uganda na Congo waliwaokoa takriban raia 200 katika uvamizi dhidi ya kambi ya magaidi mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wiki iliyopita, jeshi la Uganda lilisema Jumatatu.

Mateka hao walikuwa wakishikiliwa na kundi la kigaidi la Allied Democratic Forces linaloendesha harakati zake mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Kundi la ADF limeua maelfu ya raia mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo tangu kuzidisha mashambulizi mwaka 2014, kulingana na takwimu za Umoja wa Mataifa.

Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo limesema kundi hilo lilihusika na utekaji nyara wa raia wengi na kuwalazimisha vijana wa kike waliotekwa kuolewa.

Wengi walionekana 'dhaifu'.

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Uganda lilisema katika taarifa kwamba walioachiliwa kutoka kwenye kambi iliyo karibu na Mto Epulu ni pamoja na msichana wa miaka 14. Msemaji wa UPDF Chris Magezi aliambia Reuters uvamizi huo ulifanyika wiki jana.

"Watu kadhaa walionekana dhaifu, wakiugua magonjwa ambayo hayajatibiwa kama vile malaria, magonjwa ya kupumua, na uchovu wa kimwili," taarifa ya UPDF ilisema.

Uganda ilituma wanajeshi wake DR Congo mwaka 2021 kusaidia serikali ya Congo kupambana na ADF.

Kundi la kigaidi la ADF lilichukua silaha dhidi ya mamlaka ya Uganda katikati ya miaka ya 1990 kutoka katika kambi za magharibi mwa Uganda lakini likafurushwa mapema miaka ya 2000, na kuwalazimu wanachama wake kutoroka kuvuka mpaka na kuingia DR Congo.

CHANZO:reuters