Ryder alisema watakutana karibuni kujadili swala la kuondoka kwa jeshi la Marekani Niger. / Picha: AA

Maafisa wa Marekani wanapanga kukutana na wajumbe wa serikali ya Niger kuhusu kuondolewa kwa wanajeshi wa Marekani katika nchi hiyo ya Kiafrika, alisema msemaji wa Pentagon.

"Kulingana na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, Balozi wa Marekani nchini Niger Kathleen FitzGibbon na Meja Jenerali Kenneth Ekman, Mkurugenzi wa Mkakati, Ushirikiano na Mipango wa Marekani barani Afrika, watakutana na Kamati ya Kitaifa ya Kulinda Maofisa wa Nchi (CNSP) Aprili 25 huko Niamey, Niger kuanzisha majadiliano juu ya uondoaji kwa utaratibu na salama wa vikosi vya Marekani kutoka Niger," Meja Jenerali Patrick Ryder alisema Jumatano katika taarifa.

Christopher Maier, Katibu Msaidizi wa Ulinzi wa Operesheni Maalum na Migogoro ya Kiwango cha Chini, na Luteni Jenerali Dagvin Anderson, Mkurugenzi wa Wafanyakazi wa Pamoja wa Maendeleo ya Kikosi cha Pamoja, watafanya mikutano ya kufuatilia katika mji mkuu Niamey wiki ijayo, Ryder aliongeza.

Marekani ina takriban vikosi 1,100 nchini Niger.

Niger inatawaliwa na baraza la majeshi ambayo ilimuondoa madarakani Rais mteule Mohamed Bazoum Julai mwaka jana, ikitoa sababu ya hali mbaya ya usalama.

Nchi hiyo ya Afrika Magharibi ilisitisha makubaliano yake ya muda mrefu ya kijeshi na Washington mwanzoni mwa mwezi Machi mwaka huu, na kutangaza kuwepo kwa wanajeshi na wakandarasi wote wa Marekani kuwa ni "haramu" kwa sababu "haikuidhinishwa kidemokrasia, na ukosefu wa uwazi kuhusu shughuli za kijeshi," alisema msemaji wa serikali ya Niger Amadou Abdramane.

Wakati wa serikali za awali nchini Niger, wanajeshi wa Marekani walitoa mafunzo kwa vikosi vya Niger kukabiliana na ugaidi.

TRT World