Bei ya juu ya mafuta nchini Kenya kwa kiasi inatokana na ushuru mkubwa, kulingana na Wakenya wengi. / Picha: AFP

Bei ya petrol nchini Kenya kwa kipindi cha Novemba 15 hadi Desemba 14, 2023, inabakia bila mabadiliko, wakati bei za diesel na kerosene zimepungua kwa Ksh2.00 kila moja ($0.013) kwa lita ya bidhaa hizo.

Mamlaka ya Nishati na Udhibiti wa Petroli ya Kenya (EPRA) ilitangaza Jumanne kuwa gharama ya wastani ya petrol iliyoshushwa iliongezeka kwa 2.81%, wakati diesel iliongezeka kwa 3.28%. Kwa upande mwingine, kerosene (mafuta ya taa) iliongezeka kwa 6.31%.

"Ili kuzuia watumiaji kutokana na ongezeko la bei katika vituo vya mafuta kama matokeo ya kuongezeka kwa gharama ya bidhaa, serikali imechagua kudhibiti bei za mafuta kwa mzunguko wa bei wa Novemba-Desemba 2023," EPRA ilisema.

"Hazina ya Kitaifa imepata rasilimali ndani ya mfuko wa sasa wa rasilimali kufidia kampuni za uuzaji mafuta," EPRA iliongeza.

Miongozo ya bei

Kenya inaagiza bidhaa zake zote za petroli katika hali iliyosafishwa, EPRA ilisema.

Kufuatia sahisho la hivi punde, lita moja ya petroli katika mji wa bandari wa Mombasa, ambapo mafuta hutua inaposafirishwa, inasalia kuwa Ksh214.30 ($1.41). Dizeli itauzwa kwa Ksh200.41 ($1.32), huku mafuta ya taa yatauzwa kwa Ksh199.99 ($1.32).

Katika jiji kuu la Nairobi, lita moja ya petroli chini ya mwongozo mpya wa bei ya pampu ni Ksh217.36 ($1.47), dizeli Ksh203.47 ($1.34) na mafuta ya taa Ksh203.06 ($1.34).

Bei za mafuta jijini Nairobi zinakaribia kufanana na gharama za mji wa tatu wa Kisumu nchini Kenya, mji wa nne wa Nakuru, na mji mkuu wa Rift Valley, Eldoret.

Mandera, kaunti iliyo karibu na mpaka wa Kenya na Somalia na iko kilomita 1,025 kaskazini mashariki mwa jiji kuu la Nairobi, ina bei ya juu zaidi ya mafuta chini ya uhakiki mpya wa EPRA, huku lita moja ya petroli ikiuzwa Ksh231.36 ($1.52), dizeli Ksh217. 47 ($1.43) na mafuta ya taa Ksh217.06 ($1.43).

Afueni kwa Wakenya

Bei ya mafuta nchini Kenya kwa mara ya kwanza ilivuka alama ya Ksh200 ($1.32) katika ukaguzi wa Septemba 14, 2023.

Bei zilizodumaa sasa zinaleta afueni kwa Wakenya, ambao walikuwa wakihofia kwamba gharama zinaweza kuongezeka baada ya Waziri wa Nishati Davis Chirchir kusema mapema Novemba kwamba mzozo kati ya Israel na Hamas unaweza kuongeza gharama ya mafuta kimataifa.

TRT Afrika