Takriban wanamgambo 40 wa Al-Shabaab waliuawa mnamo Julai 9, 2023 nchini Somalia wakati wa uvamizi wa alfajiri, wizara ya ulinzi ya nchi hiyo ilisema. Picha: AP 

Takriban watu 40 wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa Al-Shabaab wameuawa katika eneo la kusini mwa Somalia.

Wizara ya Ulinzi ya Somalia ilisema Jumapili waliouawa wakati wa mashambulizi ya angani na ardhini na Jeshi la taifa la Somalia (SNA) ni pamoja na viongozi wa kundi hilo la wanamgambo,

Washukiwa wa wanamgambo walivamiwa katika mji wa Welmaro, kilomita 40 kutoka Afmadow katika eneo la Lower Jubba, Shirika la Habari la Kitaifa la Somalia (SONNA) linaripoti.

Mashambulizi ya Jumapili alfajiri yalilenga maficho ambapo washukiwa wa wanamgambo wa Al-Shabaab walikuwa wanajipanga.

Jeshi la Somalia, katika juhudi za pamoja na wanajeshi wa kimataifa, liliharibu maficho, ghala la silaha na kuwaua washukiwa 40 wa wanamgambo, "wakiwemo viongozi kadhaa wa vyeo vya juu."

TRT Afrika na mashirika ya habari