Mfalme wa falme ya Busoga nchini Uganda Kyabazinga Kyabazinga William Wilberforce Gabula Nadiope IV amefunga ndoa  na Jovia Mutesi / Picha kutoka Kyabazinga wa Busoga 

Busoga ni mojawapo ya falme nne za makatiba ya Uganda. Eneo la Busoga linapatikana mashariki mwa Uganda. Mji mkuu wa ufalme wa Busoga ni Bugembe, karibu na Jinja (mji wa pili kwa ukubwa nchini Uganda, baada ya Kampala).

Ufalme wa Busoga ni taasisi ya kitamaduni ambayo inalenga ushirikishwaji na umoja miongoni mwa watu wa eneo la Busoga ambayo inapatikana kupitia mpango wa maendeleo ili kuboresha hali yao ya maisha.

Kyabazinga wa sasa wa Busoga ni William Kadhumbula Gabula Nadiope IV/ Picha kutoka Kyabazinga wa Busoga 

Mfalme wa Busoga anaitwa 'Isebantu Kyabazinga' ikiwa Kyabazinga wa sasa ni William Kadhumbula Gabula Nadiope IV aliyezaliwa mwaka 1988.

Isebantu maana yake ni "baba wa watu."Jina hili lilikuwa ishara ya umoja huku watu wa Busoga wakitambua kuwa kiongozi wao alikuwa "baba wa watu wote ambaye huwaleta wote pamoja," na ambaye pia hutumika kama kiongozi wao wa kitamaduni.

Harusi ilihudhuriwa na mtoto wa rais wa Uganda, jenerali Muhoozi Kainerugaba 

Kuwa Kyabazinga huko Busoga ni wadhifa uliochaguliwa.

Hapo awali, Kyabazinga alichaguliwa kutoka miongoni mwa machifu watano wa urithi ambao wanafuatilia nasaba zao moja kwa moja kutoka Bunyoro-Kitara.

Katiba ya Busoga sasa imefanyiwa marekebisho kuruhusu machifu wote 11 wa urithi kugombea nafasi ya Kyabazinga.

Mara ya mwisho ufalme wa Busoga ulikuwa na harusi ya kifalme ilikuwa mwaka 1956 photo by Kyabazinga of Busog

Ufalme wa Busoga una raia wapatao milioni mbili ambao wanaishi katika maeneo 11 ya eneo la Busoga.

Harusi ya Busoga ilihudhuriwa na wananchi kutoka maeneo tofauti ya Busoga / Picha ya Kyabazinga wa Busoga

Harusi hii ilikuwa wakati wa majivuno kwa watu wa Busoga na walijitokeza kwa wingi kuhudhuria sherehe hii ya kihistoria,

Mara ya mwisho ufalme wa Busoga ulikuwa na harusi ya kifalme ilikuwa mwaka 1956 wakati Henry Wako Muloki alimuoa Alice wako Muloki.

TRT Afrika