Jaji apigwa risasi na afisa wa polisi anayesemekana alikuwa mume wa mshtakiwa / Picha: Wengine 

Tukio la ufyatuaji risasi likihusisha afisa wa polisi na hakimu limetokea katika mahakama ya Makadara jijini Nairobi nchini Kenya.

"Wakati wa kikao cha wazi cha mahakama leo hakimu alifuta dhamana kwa mshtakiwa ambaye aliruka bondi na kushindwa kutoa maelezo ya kuridhisha ya kuruka bondi. Uamuzi huu ulitamkwa, mtu alimpiga risasi hakimu na kumjeruhi kwenye mguu," taarifa kutoka mahakamani imesema.

"Maofisa wa polisi katika eneo la tukio walijibu na kumkata makali mpiga risasi huyo na hakimu wa mahakama akakimbizwa hospitali kwa matibabu. Taarifa za awali zinaonyesha kuwa aliyempiga risasi ni afisa wa polisi ambaye amekamatwa na mtuhumiwa," ripoti hiyo imeongezea.

TRT Afrika