| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Raia wa Marekani waokolewa baada ya mashambulizi katika kambi ya mbuga ya wanyamapori Msumbiji
Msumbiji imekuwa ikikabiliana na ugaidi katika mkoa wa kaskazini wenye utajiri wa gesi wa Cabo Delgado tangu 2017, mapigano yaliyosababisha vifo vya maelfu ya watu na maelfu wengine kuondoka kwenye makazi yao.
Raia wa Marekani waokolewa baada ya mashambulizi katika kambi ya mbuga ya wanyamapori Msumbiji
Ubalozi wa Marekani nchini Msumbiji unasema kuwa unafahamu kuhusu shambulio hilo karibu na Hifadhi ya Niassa. Picha: Wengine

Wamarekani wasiopungua watatu waliokolewa baada ya wanaoshukiwa kuwa magaidi kuvamia kambi ya eneo la wanyamapori kaskazini mwa Msumbiji, kulingana na chanzo kilichoshuhudia tukio hilo.

Shirika la habari la Msumbiji la Zitamar, liliripoti tukio hilo siku ya Alhamisi, kubaini huenda kulikuwa na watu waliofariki.

Mchambuzi wa kanda Tertius Jacobs anasema anaamini kuwa magaidi wamewateka raia kadhaa. Taarifa zote hazikuweza kuthibitishwa.

Msumbiji imekuwa ikikabiliana na ugaidi katika mkoa wa kaskazini wenye utajiri wa gesi wa Cabo Delgado tangu 2017, mapigano yaliyosababisha vifo vya maelfu ya watu na maelfu wengine kuondoka kwenye makazi yao.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani anasema Ubalozi wa Marekani nchini Msumbiji ulikuwa na taarifa kuhusu hoteli hiyo ilioko karibu na Hifadhi ya Niassa, karibu na Cabo Delgado, lakini hakuthibitisha kama kuna raia wowote wa Marekani waliohusika.

Chanzo hicho, ambacho hakikutaka kutambuliwa kutokana na namna suala hilo lilivyo nyeti, kinasema eneo hilo lilichomwa moto lakini hakuna thibitisho la watu wangapi waliouawa. Chanzo hicho kinasema raia watatu wa Marekani walikuwa wanawinda wakati shambulizi hilo lilipotokea, na kwamba wafanyakazi wa sehemu hiyo walikimbia wakati wanajeshi wa Msumbiji walipofika kusaidia.

CHANZO:TRT Afrika Swahili