Nigeria imeomba radhi kwa mamlaka za Afrika Kusini kufuatia kusimikwa kwa raia mmoja wa Nigeria kama "mfalme" katika mkoa wa Eastern Cape nchini Afrika Kusini.
Chifu Solomon Ogbonna Eziko alisimikwa kama "Igwe Ndigbo Na eneo la East London", kumaanisha mtawala wa kijadi wa jamii ya Waigbo ya East London, mji katika mkoa wa Eastern Cape nchini Afrika Kusini, Machi 14, 2026.
Hili lilisababisha shutuma kutoka kwa wakazi na mamlaka za Afrika Kusini, ambao waliona ni kama "kutoheshimu" sheria za Afrika Kusini na mila za jamii ya eneo hilo.
Wito wa utulivu
Kumekuwa na wito wa kuwa na utulivu na mamlaka. Ubalozi wa Nigeria nchini Afrika Kusini, ambao umejitenga na kusimikwa huko, umewashauri raia wa Nigeria kuingatia usalama wao.
Kaimu Naibu Balozi Olajide Ogunmadeji pia aliomba radhi kwa niaba ya Nigeria kwa taasisi za kijadi za Afrika Kusini, akisisitiza kuwa Ubalozi ulikuwa unawasiliana na mamlaka za Afrika Kusini kutatua tatizo hilo.
"Tunaomba radhi kwa kile kilichotokea. Ubalozi kamwe, kwa vyovyote vile, kuunga mkono kudunishwa kwa taasisi za kijadi. Hapana, hatuwezi kufanya hivyo," Ogunmadeji amesema, kulingana na shirika la habari la taifa la Afrika Kusini SABC.
Raia wa Nigeria wanaoishi Afrika Kusini pia wameomba radhi wakisema kuwa kusimikwa kwa kiongozi wa Igbo hakukueleweka.









