| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Watu 9 wamefariki baada ya basi la abiria kuigonga treni ya mizigo nchini Zimbabwe
Watu wengine 25 wamejeruhiwa baada ya dereva wa basi kushindwa kusimama na kuruhusu treni kupita, mamlaka zimesema.
Watu 9 wamefariki baada ya basi la abiria kuigonga treni ya mizigo nchini Zimbabwe
Ajali hiyo imetokea siku kadhaa baada ya basi dogo lililokuwa limewabeba wanafunzi kuchomeka. / / AA

Watu tisa, wakiwemo watoto wawili, wamefariki dunia huku wengine 25 wakijeruhiwa baada ya basi la abiria kuigonga treni ya mizigo kusini mwa Zimbabwe siku ya Jumanne, kwa mujibu wa mamlaka ya nchi hio.

“Ajali hio imetokea kwenye Barabara ya Mbizi katika eneo la Triangle, wilaya ya Chiredzi, wakati basi la Makuku lililokuwa likisafiri kutoka Chikombedzi kwenda Masvingo lilipoingia kwenye njia ya treni ya mizigo iliyokuwa ikija,” msemaji wa Shirika la Reli la Taifa la Zimbabwe, Andrew Kanambura, alisema katika taarifa iliyotumwa kwa wanahabari kupitia barua pepe.

Aliongeza kuwa dereva wa basi alishindwa kusimama na kuhakikisha hakuna treni inayokuja kabla ya kuvuka njia ya reli, jambo ambalo ni ukiukaji wa kanuni za usalama wa reli.

Msemaji wa Polisi wa Taifa wa Zimbabwe, Paul Nyathi, alisema kuwa waliofariki ni watu wazima saba na watoto wawili, huku majeruhi wakipelekwa hospitalini kupokea matibabu.

“Maelezo zaidi yatatolewa hivi karibuni, maafisa wa polisi bado wanaendelea kushughulikia ajali hiyo,” alisema Nyathi.

Ajali hiyo imetokea chini ya wiki moja baada ya basi dogo lililokuwa limewabeba wanafunzi kushika moto katikati mwa Zimbabwe, na kusababisha vifo vya watoto saba.

CHANZO:AA