| Swahili
ULIMWENGU
1 DK KUSOMA
Korea Kusini: Bunge lapitisha kura ya kutokuwa na imani na Rais
Mamlaka na majukumu ya urais ya Yoon yatasitishwa baada ya nakala za hati kuhusu mashtaka kuwasilishwa kwake na kwa Mahakama ya Kikatiba.
Korea Kusini: Bunge lapitisha kura ya kutokuwa na imani na Rais
Wabunge 204 katika bunge la Korea Kusini walipiga kura kumshtaki Rais Yoon. / Picha: AP / Others
14 Desemba 2024

Bunge la Korea Kusini limepiga kura kutokuwa na imani na Rais Yoon Suk Yeol kuhusu tamko lake la muda mfupi la sheria ya kijeshi mwezi huu.

Bunge la Kitaifa lilipitisha hoja hiyo kwa kura 204-85 siku ya Jumamosi.

Mamlaka na majukumu ya urais ya Yoon yatasitishwa baada ya nakala za hati kuhusu mashtaka kuwasilishwa kwake na kwa Mahakama ya Kikatiba.

Mahakama ina hadi siku 180 kuamua ikiwa itamfukuza Yoon kama rais au kurejesha mamlaka yake. Iwapo ataondolewa afisini, uchaguzi wa kitaifa wa kuchagua mrithi wake lazima ufanywe ndani ya siku 60.

Pata habari zaidi kupitia Whatsapp channels

CHANZO:TRT World