Fidan alisema ushindani kati ya China na Marekani unatazamiwa kuongezeka, akimaanisha ushindani wa kiuchumi kati ya mataifa hayo mawili. / Picha: AA

Waziri wa mambo ya nje Hakan Fidan ameonya kuwa Uturuki na eneo hilo lazima wawe tayari kwa vita vinavyoweza kutokea kati ya Israeli na Iran kwa sababu kuna "uwezekano mkubwa" wa kuzuka.

"Vita kati ya Israeli, Iran vinahitaji kuchukuliwa kuwa ni uwezekano mkubwa," Fidan alisema kwenye kipindi cha televisheni siku ya Alhamisi.

"Ninaamini kwamba kutathmini hii kama uwezekano mkubwa na mataifa ya kikanda itakuwa hatua ya busara zaidi, kwani tunahitaji kuwa tayari kwa hali kama hiyo, kama nchi na kama kanda. Kuenea huku kwa hakika si jambo tunalolitaka. Kuenea kwa vita katika kanda na kuchochea kwa maeneo yasiyo na utulivu sio kile tunachokihitaji," aliongeza.

Uturuki haiungi mkono "mgogoro wowote na Iran ambao unaweza kuzidi kuwa vita," alisema Fidan, na kuongeza kuwa Ankara inapinga kabisa hilo, huku akibainisha kuwa Tehran ina haki ya kujilinda ikiwa Iran itatumia haki hiyo.

Akigusia sera za kigeni na usalama za Uturuki, Fidan alisema Uturuki "haikutupia macho hata inchi moja ya ardhi ya mtu yeyote na inalenga kufanya uhusiano zaidi kupitia maendeleo ya kikanda, utulivu na ustawi."

Fidan alisema ushindani kati ya China na Marekani unatazamiwa kuongezeka, akimaanisha ushindani wa kiuchumi kati ya mataifa hayo mawili.

'Makaburi ya wazi'

Kuhusu madai cha kifo cha Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Hamas, Yahya Sinwar, Fidan alisema kwamba Ankara inasubiri uthibitisho kutoka kwa Hamas, na kuongeza kuwa hakuna kanusho lililopokelewa hadi .

"Gaza kwa bahati mbaya imegeuka kuwa makaburi ya wazi ambapo maelfu ya watu wasio na hatia wameuawa na kutendewa mauaji ya halaiki," alisema.

Akibainisha kuwa Ankara ilitathmini Israeli kuwa "katika mpango wa hatua za kijeshi ili kuondoa moja baada ya nyingine vitisho vinavyoikabili, ikiwa ni pamoja na Hamas, Hezbollah, Houthis nchini Yemen, na mambo mengine," alielezea nia ya Uturuki ya kuzuia kufunguliwa kwa mlango mwingine wa vita.

Akisisitiza kwamba nchi za kikanda hazionyeshi uhisia sawa na Lebanon kama zinavyoonyesha Palestina, Fidan alisema: "Kuna msimamo huko. Msimamo huu bila shaka ni wa maana na wa kina. Tunahitaji kuangalia sababu zilizo nyuma yake."

TRT World