Erdogan alimtakia kila la heri Muhammad Yunus katika jukumu lake jipya, akiangazia uhusiano thabiti na Bangladesh. / Picha: AA

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ametuma salamu za rambirambi kwa kiongozi wa serikali ya mpito ya Bangladesh kutokana na mafuriko yaliyosababisha vifo vya watu katika nchi hiyo ya Kusini mwa Asia.

Kupitia njia ya simu siku ya Jumanne, Rais Erdogan alisema kuwa "Uturuki inasimama, kama kawaida, na watu wa Bangladesh katika mapambano yao dhidi ya maafa na uponyaji wa majeraha."

Rais Erdogan na Muhammad Yunus pia walijadili uhusiano wa nchi mbili, na masuala ya kikanda na kimataifa, Kurugenzi ya Mawasiliano ya Uturuki ilisema kwenye mtandao wa X.

Akibainisha kuwa Uturuki na Bangladesh zinaendelea kuboresha ushirikiano wao katika maeneo yote, rais wa Uturuki alielezea kwamba anatarajia uchaguzi utakaoandaliwa na serikali ya mpito utaweza kusababisha "matokeo mazuri" kwa watu wa Bangladesh.

Zaidi ya hayo, Erdogan alimtakia kila la heri Muhammad Yunus katika jukumu lake jipya, akiangazia uungaji mkono wa Uturuki na ukuzaji wa uhusiano thabiti na Bangladesh.

Zaidi ya watu milioni 5 wameathirika na mafuriko

Mafuriko ya hivi majuzi yamegharimu maisha ya watu 23 mashariki mwa Bangladesh, na kuwalazimu maelfu kutafuta makazi, kulingana na ripoti za vyombo vya habari vya ndani.

Maji ya mafuriko yanapopungua polepole, idadi kubwa wa watu milioni 5.7 walioathirika wanasalia kutengwa na wanahitaji chakula cha haraka, maji safi, dawa na nguo, juu ya yote hayo, maeneo ya mbali ambapo barabara zimefungwa zimezuia juhudi za uokoaji na misaada.

Idara ya Hali ya Hewa ya Bangladesh ilisema kuwa hali ya mafuriko inaweza kuendelea ikiwa mvua za masika zitaendelea kunyesha, kwani viwango vya maji vinapungua polepole sana.

Takriban watu 470,000 wamekimbilia katika makazi 3,500 katika wilaya zilizokumbwa na mafuriko, ambapo karibu timu 650 za matibabu ziko uwanjani kutoa matibabu, pamoja na jeshi, jeshi la anga, jeshi la wanamaji, na walinzi wa mpaka wa nchi ya Asia Kusini wakisaidia katika uokoaji na shughuli za misaada, mamlaka ilisema.

TRT World