Katika hotuba yake, Erdogan pia alisisitiza kuwa Uturuki "haiwezi kuwekwa katika kambi moja kutokana na uhusiano wake wa kijiografia, kibinadamu, kiuchumi na kihistoria." / Picha: AA

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amewakosoa washirika wa Uturuki katika muungano NATO, kwa kutounga mkono juhudi za nchi hiyo za kukabiliana na ugaidi dhidi ya kundi la kigaidi la PKK.

"Unaweza kuona kwamba silaha tunazopewa kwa kusita na washirika wetu zinapatikana katika makao ya shirika la kigaidi linalotaka kujitenga la (PKK)," Erdogan alisema katika taarifa yake kwenye Mkutano wa Baraza la Mawaziri, Jumanne.

Kauli hiyo ilitolewa katika hotuba ya Erdogan kwa mkutano wa viongozi wa NATO wiki iliyopita, kuadhimisha miaka 75 ya muungano huo, ambapo alilaani uhusiano uliokuzwa na baadhi ya wanachama wa NATO na PKK.

"Hatuwezi kukubali uhusiano potofu ambao baadhi ya washirika wetu wameanzisha na PYD-YPG, tawi la kundi la kigaidi la PKK huko Syria ," alisema siku ya Ijumaa kupitia mtandao wa X, akihimiza ya kwamba kutoheshimu sera zinazodhuru umoja na mshikamano wa NATO.

Katika kampeni yake ya ugaidi ya takriban miaka 40 dhidi ya Uturuki, PKK - iliyoorodheshwa kama kundi la kigaidi na Uturuki, Marekani, na EU - imehusika na vifo vya zaidi ya watu 40,000, ikiwa ni pamoja na wanawake, watoto na watoto wachanga.

'Hatugeuzi mgongo wetu dhidi ya Mashariki'

Katika hotuba yake, Erdogan alisisitiza kuwa Uturuki "haiwezi kuwekwa katika kambi moja kutokana na uhusiano wake wa kijiografia, kibinadamu, kiuchumi na kihistoria."

"Hatuwezi kuruhusu wengine kutuwekea mipaka kwa mifumo yao midogo. Hatuigeuzii migongo yetu dhidi ya Mashariki kwa kupendelea Magharibi, wala hatuipuuzi Magharibi kwa kupendelea Mashariki.”

Rais wa Uturuki pia alitoa wito wa masuluhisho ya amani kwa mizozo kwa njia ya majadiliano na mazungumzo ya pande zote, akielezea kuwa ni "manufaa kufungua ngumi zilizokunjwa."

Kuhusu vita vya kikatili vya Israel dhidi ya Gaza huko Palestina, ambayo sasa imeingia siku ya 284, Erdogan alikuwa wazi kabisa: "Maadamu sera ya Israel ya mauaji, ukaaji, na mauaji ya halaiki huko Gaza na maeneo mengine ya Palestina yanaendelea, hatutabadilisha msimamo wetu kuhusu nchi hii."

Rais alisisitiza uungaji mkono usioyumba wa Uturuki kwa Palestina, na kuongeza kuwa Israeli na washirika wake "wanajiilisha damu, machozi na uvamizi."

TRT World