Wanariadha wa Afrika wanaotarajiwa kung'ara katika mbio za marathoni Boston

Wanariadha wa Afrika wanaotarajiwa kung'ara katika mbio za marathoni Boston

Mnamo 2023, mbio za marathoni za Boston zitafanyika kwa mara ya 127
Berlin Marathon / Photo: Reuters

Kevin Phillips Momanyi

Mashindano ya kila mwaka ya marathoni hii kubwa zaidi duniani yatavuta baadhi ya wanariadha wa juu wa mbio ndefu kwenye jiji la Massachusetts.

Eliud Kipchoge

Eliud Kipchoge | Photo: Reuters

Eliud Kipchoge, nyota wa marathoni mwenye umri wa miaka 36, atajaribu kushinda shindano hilo kwa mara ya kwanza. Kwa sababu hii, alijiondoa kwenye mbio za London Marathon za Aprili 29. Ameshinda huko Berlin, London, Chicago, na Tokyo, bado tu New York na Boston.

Mwanariadha huyu mashuhuri wa Kenya atakabiliana na mabingwa watatu wa mashindano yaliyopita. Hawa ni bingwa mtetezi, Evans Chebet, na mshindi wa 2021, Benson Kipruto. Lelisa Desisa wa Ethiopia, bingwa mara mbili (2013 na 2015) pia atashiriki mbio hizo.

Gabriel Geay

Gabriel Geay | Photo: Reuters

Gabriel Geay, mwenye umri wa miaka 26 kutoka Tanzania, anatarajiwa kuleta nguvu ya vijana kwenye mbio hizo. Geay ameshinda katika mbio saba muhimu za barabarani, zikiwemo Bolder Boulder mwaka wa 2017 na Peachtree Road Race mwaka wa 2016. Alishika nafasi ya sita mwaka wa 2021, na kuweka rekodi mpya ya kitaifa ya Tanzania kwenye Milan Marathon akitumia saa 2:04:55.

Mbio hizi za marathoni pia zitashirikisha John Koriri, Norbert Kigen, na Mark Korir, ambao wote ni washindani wa kiume kutoka Kenya. Herpasa Negasa, Shura Kitata, na Andualem Belay watachuana kwa Ethiopia, na Ghirmay Ghebreslassie kutoka Eritrea akifanikisha nambari ya washindani kutoka eneo hilo.

Amane Beriso

Onyesho la kusisimua linatarajiwa kwa mbio za wanawake pia. Anayetarajiwa kuibuka mshindi ni Amane Beriso wa Ethiopia. Tayari ameshiriki katika mbio za Boston Half Marathon mara mbili, kwa hivyo hana jipya. Rekodi yake binafsi ni saa 2, dakika 14, na sekunde 58, ambayo alifanikisha huko Valencia, Espania Desemba mwaka jana. Alipona kutokana na msururu wa matatizo ya goti mwaka jana na akashinda mbio za Mexico City Marathoni Agosti 2022.

Weldu Gebrehiwet kutoka Eritrea anaongoza orodha ya wanariadha wa kike kutoka eneo hilo, akifuatiwa na Gotytom Gebreslase, Hiwot Gebremaryam, Ababel Yeshaneh, na Atsede Baysa kutoka Ethiopia ambao wote watakuwa wakiwania tuzo hii.

Edna Kiplagat

Edna ni bingwa wa dunia wa marathoni wa mwaka 2011 na 2013 . Ameshinda mbio za Boston Marathon mara mbili. Alikua mwanamke mwenye umri kubwa zaidi aliyewahi kushinda tuzo ya Dunia ya Marathoni aliposhika nafasi ya kwanza katika Boston Marathon 2021 akiwa na umri wa miaka 41.

Edna Kiplagat | Picha: Reuters

Hellen Obiri

Hellen Obiri | Picha: Reuters

Hellen Obiri, kutoka Kenya ataingia katika mbio hizo kwa mara ya kwanza. Yeye ni bingwa wa kimataifa mara mbili. Alishinda medali ya fedha katika mbio za mita 5000 katika michezo yote miwili ya Olimpiki jijini Tokyo mwaka 2020 na Rio de Janeiro mwaka wa 2016. Baada ya kushinda mbio za mita 5000 mwaka wa 2017 na tena mwaka wa 2019, na kuweka rekodi mpya ya ubingwa.

Wanariadha wengine mashuhuri wa kike kutoka Kenya wanaoshiriki mbio hizo ni Sheila Chepkirui, Joyciline Jepkosgei, Angela Tanui, Fancy Chemutai, Edna Kiplagat, Celestine Chepchirchir, Maurine Chepkemoi, Mary Ngugi, na Vivian Chepkirui.

Macho yote sasa yanaelekezwa kwa wanariadha hao waliosafiri masafa marefu kutoka mataifa yao barani Afrika ili kukimbiza malengo yao ya kushiriki mbio za marathoni. Wacha misuli sasa ipashwe moto kwani jukwaa sasa liko tayari na kazi ngumu imekamilika!