| Swahili
MICHEZO
2 DK KUSOMA
Uingereza yaichapa Serbia, michuano ya EURO 2024
Bao la kichwa la Jude Bellingham lilitosha kuwapa vijana wa Gareth Southgate uongozi wa Kundi C.
Uingereza yaichapa Serbia, michuano ya EURO 2024
Jude Bellingham akishangilia bao lake dhidi ya Serbia kwenye michuano ya fainali za mataifa ya Ulaya (Euro) 2024 inayoendelea kutimua vumbi nchini Ujerumani./Picha: Getty / Others

Nyota wa Real Madrid Jude Bellingham aliihakikishia Uingereza alama tatu na uongozi wa kundi C kufuatia bao lake dhidi ya Serbia katika mchezo wao wa ufunguzi uliofanyika kwenye uwanja wa Veltins Arena.

Bellingham alifunga kwa kichwa katika dakika ya 13 ya mchezo huo, kufuatia kazi nzuri ya Bukayo Saka katika michuano ya fainali za mataifa ya Ulaya (Euro) 2024 inayoendelea kutimua vumbi nchini Ujerumani.

"Ni mwanzo mzuri kwangu na ninajisikia furaha kuipa timu yangu ushindi ambacho ni kitu muhimu zaidi kwa sasa," alisema Bellingham.

Hata hivyo, mchezo huo nusura uingie dosari kufuatia vurugu kati ya mashabiki wa pande hizo mbili, hatua iliyowalazimu walinda usalama kuingilia kati na kuwatenganisha.

Hapo awali, Denmark na Slovenia zilitoka suluhu ya 1-1, huku Christian Eriksen akiifungia Denmark, miaka mitatu tangu alipodondoka uwanjani kwa mshtuko wa moyo, katika mchezo wa kwanza wa kundi B wa michuano ya EURO 2020 kati ya Denmark na Finland.

Pata habari zaidi kupitia Whatsapp channels

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
Hatimaye timu ya soka ya Afrika Kusini yapata kibali cha kusafiri na kushiriki Kombe la Dunia
Timu ya Afrika Kusini katika Kombe la Dunia inakabiliwa na ugumu wa visa na 'kufedheheshwa'
Liverpool yamtimua Arne Slot kufuatia msimu wa kukatisha tamaa
Tanzania itamenyana na Senegal katika fainali ya AFCON kwa vijana chini ya miaka 17
Kwa nini Kombe la Dunia 2026 litakuwa lenye ushawishi wa kimataifa zaidi katika historia ya FIFA
Pep Guardiola atangaza kuondoka Manchester City baada ya miaka 10 ya mafanikio
Marekani yalegeza masharti ya Ebola kwa timu ya DRC katika Kombe la Dunia
Pep Guardiola aipongeza Arsenal kwa ushinidi wa EPL
Ligi ya Mabingwa ya CAF:Sundowns ya Afrika Kusini kumenyana na FAR Rabat ya Morocco katika fainali
Michael Carrick kubaki kuwa kocha wa Manchester United?
Hakuna visa za Marekani zilizotolewa kwa timu ya Iran kushiriki Kombe la Dunia la 2026
CAF imethibitisha tarehe za AFCON 2027 nchini Kenya, Tanzania na Uganda
Rais wa Kenya ampa zawadi kedekede bingwa wa marathon Sabastian Sawe
Bondia Anthony Joshua akubali pambano na Tyson Fury
Mkenya Sabastian Sawe aweka historia marathon kwa kumaliza muda wa chini ya saa mbili
Mshambulizi wa zamani wa Nigeria Eneramo afariki wakati wa mechi
Mjumbe wa Marekani anapendekeza kuiacha Iran na kuipa nafasi Italia katika Kombe la Dunia
Liam Rosenior amefutwa kazi kama meneja wa Chelsea
Alfonce Simbu wa Tanzania anyakua fedha katika mbio za Boston Marathon
Korir wa Kenya alivunja rekodi ya Boston Marathon wakati Mkenya mwenzake aishinda mbio za wanawake