Mkenya Faith Kipyegon asherekea kushinda fainali ya mita 1500 kwa wanawake na kuweka rekodi mpya ya dunia / Picha: Reuters

Faith Kipyegon wa Kenya amevunja rekodi ya dunia ya mita 1500 ya wanawake kwa kukimbia kwa muda wa 3:49.11 katika mkutano wa tatu wa Diamond League msimu huu huko Florence siku ya Ijumaa.

Kipyegon, mshindi wa medali za dhahabu za mita 1500 katika Michezo ya Olimpiki mbili zilizopita na taji la dunia la mwaka 2017 na 2022, alipunguza rekodi ya awali ya 3:50.07 iliyowekwa na Genzebe Dibaba wa Ethiopia mwaka 2015.

"Rekodi ya dunia ilikuwa akilini mwangu tangu mwaka jana, lakini nilitaka kuikaribia polepole ili kuona kilichowezekana mwaka huu," Kipyegon alisema katika ujumbe wake wa Twitter baada ya kukimbia vizuri sana siku ya Ijumaa.

Rais wa Kenya, William Ruto, alimpongeza Kipyegon kwa "juhudi kubwa, azimio na uimara".

Rekodi ya dunia inakamilisha mafanikio ya Kipyegon, ikiongezea medali zake mbili za dhahabu za mita 1500 katika Olimpiki na taji la dunia la mwaka 2017 na 2022, medali ya dhahabu ya Michezo ya Jumuiya ya Madola ya mwaka 2014, na mataji matatu ya Diamond League.

TRT Afrika