Exodus: Msanii wa nyimbo za injili kutoka Uganda ahubiria uelewa wa afya ya akili

Exodus: Msanii wa nyimbo za injili kutoka Uganda ahubiria uelewa wa afya ya akili

Exodus alifichua mnamo Machi kwamba amekuwa akipambana na msongo wa mawazo tangu 2013, baada ya kifo cha mama yake.
Exodus anasema ametiwa moyo kusaidia watu baada ya uzoefu wake wa unyogovu. /Picha: Exodus/Instagram

Na Charles Mgbolu

Mwimbaji wa nyimbo za Injili wa Uganda, George Lubega Timothy, ambaye ni mshindi wa tuzo nyingi za nyimbo za Injili, anayejulikana kwa jina la Exodus, ametoa shukrani kwa msaada aliopokea baada ya kushiriki kuhusu mapambano yake dhidi ya unyogovu.

Exodus alifichua mnamo Machi kwamba amekuwa akipambana na hali hiyo ya kiakili tangu 2013, baada ya kifo cha mama yake.

Mwanamume huyo mwenye umri wa miaka 40 aliandika kwenye Instagram kwamba anashukuru wote "waliosikia kilio changu kuhusu ufahamu wa afya ya akili nchini Uganda."

"Ninawakaribisha nyote mlio tayari kushirikiana nasi katika janga hili tunapoondoa unyanyapaa na ukimya kuhusu kuongezeka kwa ugonjwa wa akili nchini Uganda," aliongeza kwa ujumbe wake wa Instagram.

Hasara ya kusikitisha

Exodus anasema aliwachana na muziki lakini akapata faraja katika pombe na dawa za kulevya ambazo karibu ziligharimu maisha yake.

Exodus ni msanii wa nyimbo za injili wa Uganda aliyeshinda tuzo nyingi. /Picha: Exodus/ Instagram

"Matatizo yangu yalianza mwaka wa 2013 nilipompoteza mama yangu mpendwa.

Wakati huo, tuligundua alikuwa na saratani ya hatua ya nne.

Alipoaga dunia, nilipoteza kazi yangu, nyumba yangu na magari yangu," Exodus alisema katika chapisho, mwezi Machi.

Baada ya kupona, Exodus anasema sasa ametiwa moyo kusaidia wengine wanaopitia hali kama hizo.

"Niko kwenye kampeni ya kutoa ufahamu ili umma upate kujifunza afya ya akili ni nini au maswala ambayo yanahusika na wasiwasi na mawazo.

Ugonjwa wa afya ya akili

Exodus ameshinda tuzo ya msanii bora wa Kiume wa Uganda katika Groove na Olive Gospel Music Awards angalau mara 10, na ufichuzi wake kuhusu afya ya akili uliwagusa vijana wengi wa Uganda.

Kulingana na Jumuiya ya Kisaikolojia ya Amerika, Uganda imeorodheshwa kati ya nchi sita barani Afrika na viwango vya juu vya magonjwa ya unyogovu.

Wizara ya afya ya Uganda na Chama cha Wanasaha wa Uganda pia vimedokeza ta kwamba takriban Waganda milioni 14 wanaugua aina fulani ya ugonjwa wa akili.

“Watu wengi wanapitia changamoto hiyo lakini wanaogopa kufunguka kutokana na jinsi wananchi watakavyowahukumu, hasa wale wa sanaa ya ubunifu. Suala la afya ya akili ni janga la kimataifa ambalo bado hatujalikubali,” Exodus alisema.

TRT Afrika